UTOAJI WA MIKOPO KWA WANAFUNZI MWAKA 2016/2017
Baada ya kukamilisha zoezi la Uchambuzi wa maombi ya Mikopo 88,163 yaliyopokelewa hadi kufikia 11 Agosti, 2016. Jumla ya Wanafunzi wapya 20,183 wamepangiwa Mikopo. Upangaji huu umezingatia vigezo vilivyomo katika mwongozo wa  utoaji wa mikopo uliopitishwa na Bodi ya wakurgezi na kuidhinishwa na wizaya ya elimu sayannsi na teknoloji. Vigezo hivyo ni pamoja na
      I.        Vipaumbele vya  kitaifa vinavyoendana na Mpango  wa Maendeleo  wa Taifa wa Miaka mitano, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na Mafunzo ambayo yatazalisha wataalamu wanaokidhi mahitaji  ya kitaifa katika fani za kipaumbele ambazo ni;
·         Fani za Sayansi za Tiba na Afya,
·         Ualimu wa Sayansi na Hisabati,
·         Uhandisi wa  Viwanda, Kilimo, Mifugo, Mafuta na Gesi Asilia,
·         Sayansi Asilia, na
·         Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.
      i.        Uhitaji wa waombaji hususani wenye mahitaji  maalum kama vile ulemavu na uyatima
  1. Uhitaji wa waombaji wanaotoka katika familia zenye hali duni ya kimaisha
o    Wadahiliwa yatima waliopata mkopo                                                                    873
o    Wadahiliwa wenye ulemavu wa  viungo                                                                 118
o    Wadahiliwa  wahitaji wenye  mzazi mmoja                                                          3,448
o    Wadahiliwa wahitaji waliofadhiliwa na taasisis mbali mbali                                         87
o    Wadahiliwa wahitaji wanaosoma  kozi  za kipaumbele                                           6,159
o    Wadahiliwa wahitaji wanaosoma kozi zingine                                                        9,867
Jumla                                                                                                         20,183

Kiasi cha Fedha zinazohitajika
Bajeti iliyoidhinishwa kwa ajili ya ukopeshaji kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 ni shilingi bilioni 483, kwa ajili ya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza wapatao 25,717, na wanaoendelea na masomo wapatao 93, 295.
Hatua zinazofuata:
              I.        Wanufaika wote wanaopungukiwa na sifa watachunguzwa kwa ajili ya kurekebishiwa au kuondolewa katika unufaika wa mkopo
             II.        Waombaji waliwasilisha taarifa zenye upungufu, taarifa zao zitahakikiwa, na wakibainika kuwasilisha taarifa za uongo watachukuiwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kufutiwa mikopo yao
           III.        Wanufaika wote watatakiwa kuhuisha taarifa kwa kujaza dodoso. Taarifa za ziada za kiuchumi za wazazi au walezi wao zitatumika kutanua uhalisia. Wale watakaokutwa na hadhi zisizo stahili, watapoteza sifa za kuendelea kupata mikopo na kulazimika kurejesha kiasi watakachokuwa wamepokea tayari.

IMETOLEWA NA:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. sasa hivi ukizaa umtafutie na karo. nyota ya kijani muikumbuke hasa nyie mtaokosa mikopo. hakuna zali la mentali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...