TAASISI
YA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM
MAHAFALI YA
KUMI YA TAASISI
Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es
Salaam (DIT) anawatangazia wahitimu na wadau wote wa DIT kuwa Mahafali ya Kumi
ya Taasisi yamepangwa kufanyika Jumamosi tarehe 10/12/2016.
Mahafali haya yatatanguliwa na siku
ya utoaji tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao katika mwaka
wa masomo 2015/2016, sherehe ambazo zitafanyika Ijumaa tarehe 02/12/2016.
Taasisi inapenda kuwataarifu Wahitimu
wote wa mwaka wa masomo 2015/2016 yaani wahitimu wa Shahada ya Uzamili (M.Eng),
Shahada ya Kwanza ya Uhandisi (B.Eng.), na wahitimu wa Stashahada ya Uhandisi
(OD) kusoma utaratibu wa kuthibitisha kushiriki Mahafali hayo katika tovuti ya
Taasisi (www.dit.ac.tz)
“Rehersal” itafanyika Alhamisi tarehe
08/12/2016.
Wahitimu watakaoshiriki wanapaswa
kulipia joho la Mahafali Tshs 50,000/=
(kwa wahitimu wa Shahada ya Uzamili –
M.Eng) na Tshs 30,000/= (kwa
wahitimu wa Shahada ya Kwanza (B.Eng) na Stashahada (OD) katika tawi lolote la NBC kwenye akaunti namba 018101003145 na hatimaye kujisajili
kupitia tovuti ya Taasisi (www.dit.ac.tz).
Watakaoruhusiwa kushiriki Mahafali
haya ni wale tu watakaokamilisha usajili wao.
ZINGATIA: Malipo yafanyike kwa kutumia jina
kamili kama linavyoonekana kwenye orodha ya wahitimu wa mwaka 2015/16 iliyopo
kwenye tovuti ya Taasisi, namba ya usajili na madhumuni ya malipo yaani Mahafali.
Mwisho wa kujisajili ni tarehe 15 Novemba, 2016.
Atakayeona tangazo hili anaombwa
kumjulisha mwenzake.
Tangazo hili limetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano,
Taasisi ya Teknolojia
Dar es Salaam,
S.L.P 2958,
Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...