Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) anawatangazia kuwa Muhula wa kwanza wa Mwaka wa Masomo 2016/2017 utaanza rasmi tarehe 7/11/2016.  Wanafunzi wote wa Mwaka wa kwanza (OD & BEng / BTech) wanatakiwa kuripoti chuoni kuanzia siku ya Jumamosi tarehe 29/10/2016 kwa usajili na “Orientation Week” itakayofanyika kwa wiki moja kuanzia tarehe 31/10/2016. Aidha, mambo yafuatayo ni muhimu sana kuzingatiwa kwa wanafunzi wote kuelekea ufunguzi wa Chuo.

1. Usajili utafanyika kwa wiki mbili tu na mwanafunzi ambaye hatakamilisha usajili wake kwa muda huo hataruhusiwa kuingia darasani.

2. Ili mwanafunzi akamilishe usajili ni lazima alipe Ada na kuwasilisha Bank pay in slip wakati anasajiliwa.

3. Wanafunzi wa Stashahada wenye ufadhili binafsi (Private sponsored Students) watakaopata nafasi ya  Malazi katika mabweni ya Taasisi watalazimika kulipa jumla ya Tshs 990,000/- kwa mwaka na watahudumiwa kwa utaratibu maalum watakaoelekezwa baada ya kukamilisha malipo hayo.

4. Kila mwanafunzi wa mwaka wa kwanza atahitajika kuwasilisha vyeti halisi wakati wa usajili kinyume cha hapo hatasajiliwa kama mwanafunzi wa DIT.

5. Sheria zote za udahili na mitihani zitazingatiwa kama zilivyochapishwa katika Prospectus ya Taasisi kwa Wanafunzi wote wanaoendelea yaani mwaka wa Pili hadi wa Nne na KWA WANAFUNZI WAPYA WANAONZA MWAKA WA KWANZA 2016/2017 kuna nyongeza kwenye sheria hizo kwamba; Mwanafunzi atakayeshindwa  kufaulu CA (Continous Assessment) hatapewa nafasi ya mtihani wa Marudio yaani Supplementary Exam na badala yake atalazimika kuirudia hiyo “module” upya katika mwaka wa kimasomo unaofuata. 

6. Akaunti zifuatazo zitatumika kwa malipo.
Ada na gharama nyingine:  A/C. No. 0150408417800 – CRDB
Chakula na Malazi; Bima ya Afya (NHIF); DITSO Fees zilipwe zote kupitia 
A/C No. 011103005481 – NBC LTD Tawi lolote kabla ya Usajili.

7. Malipo ya Ada ni lazima yalipwe kwa angalau 50% kabla ya kujisajili.

Ofisi ya Uhusiano,
Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam,
S.L.P 2958,
Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...