Akizungumza
kwenye uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki,
Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Toyota Tanzania, Bw. Mahmood
Karimjee alisema “Uzinduzi wa jumba hilo la maonyesho unaleta zama mpya
katika safari ya Toyota Tanzania, inadhiirisha azma ya Karimjee Group
katika kutoa huduma bora kwa wateja. Wateja sasa watafaidika na huduma
zilizoboreshwa na bora zaidi kimataifa na tunatarajia watafurahia huduma
hii kwa miaka mingi ijayo”.
Jumba
hilo kubwa la magari ya Toyota yanayotumika zaidi hapa nchini
limeboreshwa kwa kuwekewa huduma nyingi za kisasa kama kumbi za mikutano
zenye vifaa vya kisasa ili kuendana na viwango vya kimataifa na
litatumika kama maonyesho ya magari ya Toyota hususani aina mpya za
magari hayo yakiwemo yale yaliyozinduliwa hivi karibuni kama Hilux pick
mpya, Fortuner SUV na Landcruiser VXR.
Kutokana
na uwekezaji huu, Toyota Tanzania imelenga kuwapatia huduma mpya na
bora wanunuzi wa magari hayo na watu wengine watakaotembelea jumba hilo
kujionea huduma na bidhaa mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.
“Kununua gari ni maamuzi muhimu na sio jambo unaloweza kulifanya kila
siku. Hivyo basi Toyota imeamua kuhakikisha kila mnunuzi wa gari anaweza
kufurahia huduma za kisasa,” alisema Karimjee.
Kufuatia
ufunguzi huo, mwakani kampuni hiyo pia itazindua kituo cha huduma baada
ya mauzo kwa lengo la kuhakikisha watumiaji wa magari hayo wanaendelea
kupata huduma zitakazofanya magari hayo yadumu katika hali nzuri kwa
muda mrefu. Vilevile kampuni hiyo itazindua kituo cha kutoa huduma za
kuzuia magari yasiharibike na pia itatoa huduma za kukodisha magari
kupitia kampuni yake ya Salute Finance Ltd.
Karimjee
alisema uzinduzi huu ni historia muhimu katika miaka 191 familia ya
Karimjee na miaka 50 ya Toyota hapa nchini kwani jumba la mwisho la
maonyesho lilizinduliwa miaka 26 iliyopita. Uzinduzi huo ulihudhuriwa na
balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida, mabalozi mbalimbali, wapenzi
wa magari ya Toyota na Meneja Mkuu wa Toyota Motor Corporation, Bw. Yu
Asano. Ambaye aliipongeza Toyota Tanzania kwa kupiga hatua hii muhimu.
Balozi wa Japan, Masaharu Yoshida akiangalia gari jipya aina ya Land Cruiser VXR wakati wa uzinduzi wa jumba la maonyesho ya magari la Kampuni ya Toyota Tanzania jijini Dar es Salaam juzi
Balozi wa Japan, Masaharu Yoshida (kushoto) akimpongeza Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Toyota Tanzania, Mahmood Karimjee wakati wa uzinduzi wa jumba la maonyesho ya magari la kampuni hiyo jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Karimjee Jivanjee, Hatim Karimjee (kushoto) pamoja na Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida (kulia) wakifatilia uzinduzi wa jumba jipya la maonyesho ya magari ya Toyota --- Kampuni ya magari ya Toyota Tanzania Limited imezindua jumba la maonyesho la kisasa kwenye makao makuu yake jijini Dar es salam ikiwa ni jitihada za kuboresha huduma kwa wateja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...