Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe na Mkurugnzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya
ya Handeni Bw. William Makufwe wamepiga marufuku ufugaji holela. Tamko hilo limetolewa
baada ya uongozi wa kijiji cha Chogo Kata ya Kabuku Ndani kuomba Mkuu wa Wilaya
na Mkurugenzi Mtendaji kuwasaidia kuondoa wafugaji waliovamia katika kijiji
chao na kuharibu mazao ya kilimo ya wananchi wa kijiji hicho.
Akizungumza na wananchi hao Mkuu wa wilaya aliwaeleza wananchi
kuwa kila sehemu kuna taratibu na sheria zake namna ya kuishi. “ni marufuku kuchunga mifugo kwenye maeneo
ya hifadhi ya misitu ya Serikali au ya Kijiji kwa maana ni kosa akipatikana mtu wa namna hiyo kamateni
peleka polisi na mimi nifahamu”alisema, na pia ni marufuku kuchukua mifugo
kwenda kuchunga kwenye shamba la
mwenzako kuwepo na mazao au hakuna ni kosa kamateni mtu wa namna hiyo peleka polisi, hata kama mwenye shamba
amekwisha vuna isipokuwa kwa idhini ya mwenye shamba pekeyake.
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni aliwaeleza
wananchi kwamba ulinzi wa mali za
Chogo ni wanachogo wenyewe, na mgogoro
wa wakulima na wafugaji ni wetu sote, Aliwaeleza kwamba walishindwa kuchukua
tahadhari mapema pindi wafugaji hao walipoingia miezi mine iliyopita kwa sababu
eneo lao lina mpango bora wa matumizi ya ardhi.
Aidha aliwaeleza wananchi kuwa,
amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji
kuleta orodha ya mifugo iliyopo kwenye maeneo yao na waeleze uwezo wa ardhi
iliyopo kuweza kuhimili idadi ya mifugo iliyopo kwa mujibu wa mpango wa ardhi
uliowekwa katika maeneo yao ili kugungua kama kunamifugo imezidi au haijazidi, “Tarehe 29/10/2016 nitapata orodha ya
Halmashauri nzima kwa kata 21 na Vijiji
91” alisema.
Mkuu wa Wilaya Mh. Godwin Gondwe akizungumza na wannchi wa kijiji cha Chogo wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akifuatiwa na Mh.Abdalla Pendeza Diwani wa Kata ya Kabuku Ndani na wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa kijiji cha chogo.
Mkuu wa Wilaya ,Mukurugenzi Mtendaji na viongozi wengine kutoka Halmashauri wakitazama moja ya eneo laKitalu cha kuoteshea miti ya malimao mkulima baada ya kupitia shamba na kuona uharibifu uliofanyika.
baadhi ya wananchi kijiji cha Chogo Kata ya Kabuku ndani.
mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya handeni akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chogo kata ya Kabuku Ndani.
Mmoja kati ya wafugaji waliopo katika kijiji cha ChogoBw. Masanja akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi na wananchi wote kwa ujumla.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Mkuu wa Wilaya ,Mukurugenzi Mtendaji na viongozi wengine kutoka Halmashauri wakitazama moja ya eneo laKitalu cha kuoteshea miti ya malimao mkulima baada ya kupitia shamba na kuona uharibifu uliofanyika.
baadhi ya wananchi kijiji cha Chogo Kata ya Kabuku ndani.
mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya handeni akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chogo kata ya Kabuku Ndani.
Mmoja kati ya wafugaji waliopo katika kijiji cha ChogoBw. Masanja akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi na wananchi wote kwa ujumla.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...