Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, akizungumza na wanufaika wa Tasaf pamoja na wananchi wa Kata ya Sandali, ambao kaya zao bado hazijaingizwa katika mpango huo.
Diwani wa Kata ya Sandali, Temeke jijini, Abel Tarimo, akitoa maelezo kuhusu masuala mbalimbali kwenye mtaa wake huo, kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, alipokuwa na mkutano na wanufaika wa Tasaf pamoja na wakazi wa maeneo hayo jana.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki (kulia), kuzungumza na wanufaika wa Tasaf pamoja na wananchi ambao kaya zao hazijaingizwa katika mpango huo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Nasib Mbaga.
Baadhi ya wanufaika wa Tasaf katika mpango wa Serikali wa kuzinusuru kaya masikini pamoja na wananchi ambao bado hawajaingizwa katika mpango huo wa maeneo ya Kata ya Mtoni, Temeke jijini Dar es Salaam jana, wakisikiliza masuala mbalimbali yaliyokuwa yakielezwa katika mkutano huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...