Meneja Mawasiliano wa Barclays Tanzania, Hellen Siria, akihojiwa na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari, wakati wa uzinduzi rasmi wa maabara ya kompyuta inayotembea itakayohudumia shule nne za sekondari katika wilaya hiyo. Mradi wa kompyuta unawezeshwa kwa kushirikiana na asasi ya PEN Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika katika Shule ya Sekondari Kijitonyama, Dar es Salaam .
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Barclays Tanzania, Aron Luhanga (wa tatu kulia), Meneja Teknolojia wa benki hiyo, Dakshit Pandya (katikati mwenye miwani), na Mkurugenzi wa asasi ya PEN Tanzania, Sharnel Deo (wa nne kulia), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maabara ya kompyuta inayotembea itakayohudumia shule nne za sekondari katika wilaya hiyo. Mradi wa kompyuta unawezeshwa kwa kushirikiana na asasi ya PEN Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika katika Shule ya Sekondari Kijitonyama, Dar es Salaam .
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Barclays Tanzania, Aron Luhanga (wa pili kulia) akikabidhi pedi za kike kwa baadhi ya wanafunzi wa shule za sekondari za Wilaya ya Kinondoni mara baada ya uzinduzi wa maabara ya kompyuta inayotembea itakayohudumia shule nne za sekondari katika wilaya hiyo. Mradi wa kompyuta unawezeshwa kwa kushirikiana na asasi ya PEN Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika katika Shule ya Sekondari Kijitonyama, Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Teknolojia wa benki hiyo, Dakshit Pandya.
Ofisa Masoko wa Benki ya Barclays, Nasikiwa Berya (wa tano kushoto), akitoa maelekezo kwa baadhi ya wanafunzi waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa maabara ya kompyuta inayotembea itakayohudumia shule nne za sekondari katika wilaya ya Kinondoni. Mradi wa kompyuta unawezeshwa kwa kushirikiana na asasi ya PEN Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika katika Shule ya Sekondari Kijitonyama, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wengine kutoka kushoto ni Meneja Mawasiliano wa PEN Tanzania, Nancy Kataraihya, Meneja Mawasliano wa Barclays, Hellen Siria na Meneja Teknolojia wa benki hiyo, Dakshit Pandya. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...