Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Benki ya United Bank of Africa (UBA), jana imetoa msaada wa viti, Magodoro, Magongo ya kutembelea na vitabu vya kujisomea kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ya shule ya sekondari ya wavulana Pugu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kutoa vifaa hivyo, Meneja wa benki hiyo nchini ,Peter Makao, amesema kuwa wamechagua kutoa vifaa hivyo katika shule hiyo kutokana na mahitaji ya watoto hao ambao wamekuwa wakisoma katika mazingira magumu.

“Vitu hivi ambavyo tumevitoa leo vitasaidia kwa kiasi kikubwa kuwapunguzia watoto hawa wenye mahitaji maalum kusoma kwa mawazo kwa kujiona kwamba wao ni sehemu hii ya shule kwa kupata mahitaji yao wote kama ilivyo kwa wengine”Amesema Makao 

Ametoa wito kwa wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili waweze kufanikiwa katika jamii na baadae wajivunie kuwa walisoma pugu .
Wanafunzi wa Pugu sekondari wakishusha kwenye gari vifaa vilivyokabidhiwa na benki ya UBA kwa ajili ya wanafuzni wenye mahitaji maalum
Mkurugenzi mkuu wa Benki ya UBA,Peter Makao akiwa na Meneja Operesheni Omary wakikabidhi mafuta ya ngozi kwa kijana mwenye ulemavu wa ngozi ,Daudi Nyangusi na Meneja ufadhili wa eleimu kutoka TEA , Tito Mganwa.
Mkurugenzi mkuu wa Benki ya UBA,Peter Makao akiwa meneja operesheni Omary wakikabidhi vitabu kwa wanafunzi Salum Mohamed na Ramadhani Juma pamoja na Meneja ufadhili wa eleimu kutoka TEA , Tito Mganwa.
Wafanyakazi waUnited Bank of Afrika wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenye ulemavu wa shule ya Sekondari ya wavulana pugu jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...