Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB),
Abdul Razaq Badru akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wadaiwa sugu katika
mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari, MAELEZO leo Jijini Dar es
Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaadizi wa Mawasiliano wa Bodi hiyo Bw. Cosmas
Mwaisobwa.
Na: Frank Shija, MAELEZO
Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kupewa notisi ya siku thelethini
(30) wawe wameanza kulipa madeni yao kabala hatua zaidi hazijachukuliwa dhidi yao.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa
Elimu ya Juu (HESLB) Abdul – Razaq Badru alipokuwa akiongea na waandishi wa
habari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO kuhusiana na wadai sugu leo Jijini
Dar es Salaam.
Badru amesema kuwa notisi hiyo inawalenga wanufaika wa waliokopeshwa na muda
wa mataraji ukapita bila wao kuwasilisha taarifa zao na kulipia madaeni ya mikopo ya
eleimu ya juu waliyokopeshwa tangu mwaka wa masomo 1994/95.
Alisema kuwa jumla ya wanufaika 93,500 walinbainika na kupelekewa Ankara ya
madeni yao ili waweze kulipa hata hivyo kati yao ni wadaiwa 81,055 ndiyo
wanaendelea kulipa madeni yao.
Aidha Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa wapo wadaiwa sugu takribani 142,470 wenye
mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 239 hawajajitokeza wala kuanaza
kulipa mikopo yao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Urejeshaji Mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya
Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Dkt. Abdul Mussa amesema kuwa urejeshaji wa
mikopo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 jumla ya shilingi bilioni 25 zimerejeshwa hadi
kufikia mwezi Oktoba mwaka huu.
Hatua hii ya kutoa notisi ndani ya siku thelathini inafuatia kutokana na kuvunjwa kwa
sheria namba ya 19A (1) cha sheria za Bodi ya Mikopo Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa
Elimu ya Juu (HESLB) ambapo pamoja na hatua hiyo Bodi imeazimia kuchukua hatua
nyingi za ziada.
Hatua hizo ni pamoja na kuyatangaza majina ya wadaiwa sugu hadharani ili waajiri,
wadhamini wao na wadau wengine wenye taarifa za wasugu waziwasilishe,kuwasilisha
majina ya wadaiwa kwenye taasisi zinazotunza taarifa za ukopaji na kukamilisha
taratibu za kuwafikisha mahakamani kwa hatua za kisheria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...