Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko John Maige ( kushoto) akiwafafanulia jambo wadau wa kilimo cha mahindi wa Taasisi ya Bassotu Farmers Association (BFA) ya mjini Katesh , Wilaya Hanang,Mkoa wa Manyara kuhusu ubora wa unga wa mahindi wa chapa ya ‘Nguvu’ unaozalishwa na Bodi hiyo kwa kutumia kinu chake cha Iringa ,walipo mtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo ( wapili kutoka kushoto) ni Emmanuel Hhau, Joseph Malela , Haladius Philipo na kulia ni Dkt.Wilbard Lorri. Bodi hiyo iko chini ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Wadau wa kilimo cha mahindi wa Taasisi ya Bassotu Farmers Association (BFA) ya mji wa Katesh katika Wilaya Hanang mkoa wa Manyara ( wapili kutoka kushoto) Emmanuel Hhau, Joseph Malela , Haladius Philipo na kulia ni Dkt.Wilbard Lorri wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa bodi ya Nafaka na mazao mchanganyiko John Maige (kushoto) wakiwa na viroba vya unga wa mahindi wa kilo tano wa chapa ya ‘Nguvu’ unaozalishwa na bodi hiyo kwa kutumia kinu chake cha Iringa ,wakati walipomtembelea ofini kwake jijini Dar es Salaam leo . Bodi hiyo iko chini ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...