Na Teresia Mhagama.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani amezindua mradi wa umeme wa Kilowati 430 unaotokana na maporomoko ya maji katika Kata ya Ikondo mkoani Njombe ambapo mpaka sasa zaidi ya wateja 1140 wameunganishiwa umeme huku zoezi hilo likiwa ni endelevu.

Uzinduzi huo uliofanyika katika Kata  hiyo ulihudhuriwa na Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU), Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa wilaya ya Njombe, wananchi wa Kata ya Ikondo, Shirika lililotekeleza mradi huo la CEFA, watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO).

Dkt. Kalemani alisema kuwa mradi huo umetekelezwa na Taasisi isiyo ya kiserikali ya CEFA  kutoka Italia     na kugharamiwa kwa pamoja kati ya Jumuiya ya Ulaya na Serikali ya Tanzania kwa jumla ya Dola za Marekani 110,209.

Aliongeza kuwa mradi huo wa umeme utasambazwa katika vijiji vilivyoko kata za Ikondo, Matembwe na Lupembe na ziada itakayobaki inaingizwa kwenye gridi ya Taifa.

" Habari njema ni kuwa tayari vijiji Saba vimeunganishiwa umeme kupitia mradi huu, hii inatimiza moja ya malengo ya Serikali ya kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora katika maeneo ya vijijini kupitia asasi za kiraia," alisema Dkt. Kalemani.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa Mradi wa Umeme wa Maji wa Kilowati 430 katika Kata ya Ikondo mkoani Njombe.  Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Rehema Nchimbi (wa kwanza kushoto), Mbunge wa Lupembe,  Joram Hongoli (wa pili kushoto),  Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU), Jane Nunes (wa Tatu kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt Gideon Kaunda (wa pili kulia) na Balozi wa Italia nchini, Roberto Mengoni (wa Nne kulia).
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa pili kutoka kulia) akipiga makofi mara baada ya uzinduzi rasmi wa Mradi wa Umeme wa Maji wa Kilowati 430 katika Kata ya Ikondo mkoani Njombe.  Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Rehema Nchimbi (wa kwanza kushoto), Mbunge wa Lupembe,  Joram Hongoli (wa Tatu kushoto),  Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU), Jane Nunes (wa Nne kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt Gideon Kaunda (wa pili kushoto). 

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa pili kushoto) akiangalia moja ya mitambo ya kuzalisha umeme  Umeme wa Maji wa Kilowati 430 katika Kata ya Ikondo mkoani Njombe.  Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Rehema na wa kwanza kulia ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...