Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani amewataka wakazi wa mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa kuwekeza katika biashara na vivutio vya utalii ili kunufaika na fursa ya ujio wa Ndege mpya za Shirika la ndege Tanzania (ATCL) katika kanda hiyo.

Akizungumza wakati wa kuzindua usafiri wa ndege ya ATCL kutoka Kigoma kwenda Dar es salaam Eng.Ngonyani amesema Serikali itahakikisha inaufufua ukanda wa magharibi mwa Tanzania kwa kuimarisha barabara za lami na kuwa na safari za ndege za uhakika ili kuvutia watalii kutembelea vivutio hivyo na hivyo kukuza uchumi wa mikoa hiyo.

“Kwa kuanza ATCL itakuwa na safari nne kwa wiki kuja Kigoma na idadi ya abiria ikiwa ya kutosha tutaziongeza ili kuwawezesha wasafiri na wadau wengine wa utalii kufika Kigoma kwa urahisi”, Amesema Eng. Ngonyani.
Amewataka wafanyakazi wa ATCL na viwanja vya ndege nchini (TAA), kuwa wabunifu ili kuvutia abiria wengi na hivyo juhudi za Serikali za kuiunganisha nchi kwa usafiri wa  anga zifanikiwe katika muda mfupi.

“Serikali tutaendelea kuongeza ukubwa wa uwanja wa ndege wa Kigoma na Mpanda na kutoza gharama nafuu ili kuwezesha ndege nyingi kutua katika ukanda wa Ziwa Tanganyika na kuwezesha abiria na watalii wengi kunufaika na usafiri wa anga,”. Amesisitiza  Eng. Ngonyani.
 Mkuu wa Bandari ya Kigoma Bw. Athuman Mwaibamba akijadiliana jambo na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani alipoitembelea bandari ya Kigoma kukagua utendaji kazi wa bandari hiyo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akifafanua jambo kwa wafanyakazi wanaopakia na kushusha mizigo katika bandari ya Kigoma.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akisikiliza changamoto zinazowakabili abiria wanaotumia treni ya reli ya kati katika stesheni ya Kigoma.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...