Naibu Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani amewataka wakazi wa mikoa ya Kigoma,
Katavi na Rukwa kuwekeza katika biashara na vivutio vya utalii ili kunufaika na
fursa ya ujio wa Ndege mpya za Shirika la ndege Tanzania (ATCL) katika kanda
hiyo.
Akizungumza wakati wa
kuzindua usafiri wa ndege ya ATCL kutoka Kigoma kwenda Dar es salaam Eng.Ngonyani
amesema Serikali itahakikisha inaufufua ukanda wa magharibi mwa Tanzania kwa kuimarisha
barabara za lami na kuwa na safari za ndege za uhakika ili kuvutia watalii
kutembelea vivutio hivyo na hivyo kukuza uchumi wa mikoa hiyo.
“Kwa kuanza ATCL
itakuwa na safari nne kwa wiki kuja Kigoma na idadi ya abiria ikiwa ya kutosha
tutaziongeza ili kuwawezesha wasafiri na wadau wengine wa utalii kufika Kigoma
kwa urahisi”, Amesema Eng. Ngonyani.
Amewataka wafanyakazi
wa ATCL na viwanja vya ndege nchini (TAA), kuwa wabunifu ili kuvutia abiria
wengi na hivyo juhudi za Serikali za kuiunganisha nchi kwa usafiri wa anga zifanikiwe katika muda mfupi.
“Serikali tutaendelea
kuongeza ukubwa wa uwanja wa ndege wa Kigoma na Mpanda na kutoza gharama nafuu
ili kuwezesha ndege nyingi kutua katika ukanda wa Ziwa Tanganyika na kuwezesha
abiria na watalii wengi kunufaika na usafiri wa anga,”. Amesisitiza Eng. Ngonyani.
Mkuu wa Bandari ya Kigoma Bw. Athuman Mwaibamba akijadiliana jambo na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani alipoitembelea bandari ya Kigoma kukagua utendaji kazi wa bandari hiyo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akifafanua jambo kwa wafanyakazi wanaopakia na kushusha mizigo katika bandari ya Kigoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akisikiliza changamoto zinazowakabili abiria wanaotumia treni ya reli ya kati katika stesheni ya Kigoma.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...