Viongozi na wafanyakazi wa taasisi za Serikali wametakiwa kubadilika kimtazamo ili kwenda sambamba na malengo na matarajio ya Serikali ya awamu ya tano katika kukuza uchumi wa viwanda na kuongeza ajira.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani amesema Serikali imedhamiria kufufua na kuyawezesha mashirika yake yote kufanya biashara na kuzalisha faida ili kujitegemea na kuachana na utegemezi wa ruzuku toka Serikalini.

Akizungumza katika majumuisho ya ziara yake ya siku tatu mkoani Mbeya Eng. Ngonyani amezitaka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA), na Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) kubuni vyanzo vya mapato.

“Fanyeni kazi kwa ubunifu ili mzalishe faida na kuwa na uwezo wa kujiongezea mishahara na stahili mbalimbali, acheni kulalamika na kutegemea ruzuku ya Serikali katika kila jambo”. Amesisitiza Eng. Ngonyani.

Amewataka TAA kuhakikisha ndege nyingi zinautumia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe kwani ukitumika vizuri unaweza kuwa kitovu cha uchumi kwa ukanda wa kusini na nchi jirani kutokana na ubora wake.

Naibu Waziri huyo amezungumzia umuhimu wa TAZARA kutafuta soko la ndani badala ya kutegemea soko la nje pekee kwani kufanya hivyo kutapunguza mizigo mingi inayosafirishwa kwa njia ya barabara na kuhamia kwenye reli hali itakayopunguza msongamano na uharibifu wa barabara.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (wa pili kushoto), akikagua na kupata maelezo ya njia ya kuruka na kutua ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe Mkoani Mbeya, kulia kwa waziri ni Kaimu Meneja wa uwanja huo Bw. Amir Hamis.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (mwenye miwani) akikagua kifaa cha kupima kiasi cha jua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe Mkoani Mbeya.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akitoa maelekezo kwa mkandarasi DB Shapriya anayejenga jengo la abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe Mkoani Mbeya.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akikagua daraja katika reli ya TAZARA mkoani Mbeya na kusisitiza uboreshwaji wa haraka wa mazingira katika nguzo za daraja hilo ili kutoathiri daraja hilo na reli kwa ujumla.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akikagua mashine aina ya (traction motor), inayotumika kuendeshea injini ya gari moshi alipokagua karakana ya utengenezaji wa vichwa vya treni ya TAZARA Mkoani Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...