Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
SERIKALI imesema mzunguko wa fedha sio mzuri kutokana na fedha nyingi kwenda katika miradi ya kuimarisha huduma kwa wananchi.
Hayo ameyasema leo jijini Dar es
Salaam, Msajili wa Hazina, Lawlance Mafuru wakati akizungumza na waandishi
habari juu ya taarifa zinazosambaa zinazodai kuwa benki zimeyumba.
Amesema serikali katika kudhibiti
fedha za umma katika mashirika na taasisi ni kuwa na akaunti benki kuu ili
kuweza fedha hizo kuonekana na sio kuwa katika benki zingine.
Mafuru amesema kuyumba kwa taasisi za
fedha haitokani na kuondolewa kwa kiasi
cha sh.bilioni 515 kwa kila taasisi kuwa na akaunti benki kuu.
Amesema taasisi za fedha kwa septemba
zimekopesha sh.trioni 16 kati ya fedha hizo sh.trioni 1.4 ni mikopo mibovu
hivyo kwa benki lazima ziyumbe kwa muda kutokana na mikopo hiyo mibovu.
Mafuru
amesema kupanga ni kuchagua
hivyo serikali imetaka kuimarisha huduma kwa wananchi , lazima kuwekeza
kwa
kiasi kikubwa katika huduma za kijamii.Amesema viwanda vikijengwa hapa
nchini wananchi watanunua bidhaa za ndani hivyo fedha itazunguka hapa
hapa kuliko
kununua bidhaa za nje ambazo fedha zinakwenda kuwapa maendeleo nchi
nyingine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...