Na Bakari Madjeshi,Globu ya Jamii 

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imekanusha taarifa ya kutoa Zabuni kwa Kampuni ambazo hazina vigezo kupata zabuni hizo. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam,Naibu Meya wa Halmashauri hiyo,Mussa Kafana amesema kumekuwepo na taarifa ikidai kuwa Halmashauri hiyo imetoa zabuni kwa Kampuni ambazo hazina sifa. 

"Tumeona tutoe ufafanuzi kwamba hatujatoa zabuni kwa Kampuni ambayo haina sifa,Mfano Kenya Airport ambayo mpaka leo mkataba wake haujasainiwa,"amesema Kafana 

Amesema baadhi ya mikataba haijasainiwa kutokana na Kampuni hizo kutotimiza vigezo na masharti vinavyotakiwa kama zabuni inavyoeleza. 

Kafana ameeleza kuwa Mikataba haijasainiwa kutokana na Kitabu cha Zabuni kinaonyesha kuwa Halmashauri ya Jiji kitu gani inataka ikiwa ni pamoja na kutimiza Masharti hayo ya Halmashauri ya Jiji. Pia amesema Mzabuni anatakiwa kuleta dhamana ya Asilimia 10 ya kile kiwango alichobidi katika kuomba zabuni,hiyo ikiwa ni kwa mujibu wa Kitabu cha Zabuni katika sura ya 41 Kifungu cha kwanza,

Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,Mussa Kafana akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu kuwepo kwa taarifa ambayo inadai kuwa Halmashauri hiyo imetoa zabuni kwa Kampuni ambazo hazina sifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...