Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamiizi wa Mazingira Nchini,
NEMC limeipiga faini ya shilingi milioni kum na tano Halmashauri ya wilaya ya
Kahama kwa kile kinachodaiwa ni uzembe wa kuto zingatia sheria ya mazingira kwa
kuliweka Dampo la mji huo katika hali hatashi kwa mazingira na viumbe hai
wengine.
Katika Ziara ya Naibu Waziri Mpina Leo Mjini Kahama, ilohusisha
ukaguzi wa Dampo, machinjio viwanda na soko la mjini kahama kumebainika kuwa na
uzembe kwa watendaji wa Halmashauri ya mji wa Kahama, wa kutosimamia utupwaji
wa taka katika Dampo la mji huo ulohusisha kutupwa kiholela kwa taka ardhini na
kuteketezwa kwa njia isiyo salama.
Kufuatia ukiukwaji wa sheria ya mazingira ya 2004 na kanuni
zake, Baraza la mazingira nchini NEMC limeshawishika
kuitoza faini Halmashauri hiyo ya shilingi milioni kumi na tano na kutakiwa
kulipwa ndani ya wiki mbili.
Akiitaja adhabu hiyo mbele ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, Mkaguzi wa NEMC kanda ya ziwa na
Mikoa jirani Bw. Jamali Baruti sambamba na hilo ameleza kuwa, Halmashauri ya
Kahama inatakiwa kuboresha miondombi ya taka,kuratibu na kusimamia ujenzi wa
mabwawa katika machinjio mjini hapo kwani utupwaji holela wa samadi huchangia
uharibifu wa mazingira.
Akitilia msisitizo wa suala zima la uzingatiaji wa sheria ya
mazingira kwa watendaji nchini, Naibu Waziri Mpina alisema kuwa hawezi kukubali
kuwajibishwa sababu ya viongozi kushindwa kusimamia suala zima la mazingira, na
kuhaidi kuwawajibisha viongozi wazembe.
Awali, akitoa taarifa ta usafi wa mazingira ya wilaya ya Kahama
Mkuu wa Wilaya hiyo Bwana Nkulu alisema kuwa Kahama imekuwa ikikabiliwa na
chngamoto mbali mbali za kimazingira ikiwa ni Pamoja na uhaba wa magari ya
kuzolea taka, ukataji miti kwa matumizi ya kukaushia tumbaku, na usafishaji wa
dhahabu kwa kutumia madini ya zebaki ambayo si rafiki kwa mazingira.
Ziara ya Naibu Waziri
Mpina wilayani Kahama ni Muendelezo wa Ziara zake nchini za ukaguzi wa
mazingira na utekelezaji wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake.
|
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Fadhili Nkulu akitoa taarifa ya
usafi wa mazingira ya Wilaya Hiyo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais
Muunano na Maingira Mhe. Luhaga Mpina na Ujumbe wake hawapo pichani, katika
siku ya kwanza ya ziara ya Naibu Waziri Mpina
ya ukaguzi wa mazingira Wilayani Kahama.
|
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira Mhe. Luhaga Mpina mwenye T-Shirt ya mistari mnyeupe, na baadhi ya
ujumbe wake katika ziara Mjini Kahama wakiangalia sehemu ya uzalishaji wa bati
katika kiwanda cha Kahama Oil Mills ltd, kinavyokunjwa na kutoka katika
mashine, ikiwa ni siku a kwanza ya Ziara ya Naibu Waziri Mpina leo.
Kati kati mwenye t-shirt ya mistari mnyeupe, Naibu Waziri
Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina na sehemu ya
ujumbe wake katika ziara ya ukaguzi wa DAMPO la Busoka Wilayani Kahama Leo.
Sehemu ya taka ngumu zilizotupwa kiholela katika kiwanda cha
kutengeneza mafuta yatokanayo na pamba cha
Kahama Oil Mills Ltd, cha Mjini Kahama chenye kukabiliwa na changamoto
ya utengaji, utunzaji na utupaji taka ngumu kiholela kiwandani humo ambapo
Naibu Waziri Mpina alikitembelea Leo. (Habari na Picha na
Evelyn Mkokoi wa OMR)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...