Naibu Waziri
Jaffo ametoa kauli hiyo alipokuwa akifungua mafunzo ya Sheria ya Manunuzi ya
Umma inayoendeshwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa
Maafisa Masuhuli, Wenyeviti wa Bodi za Zabuni, Wakuu wa Vitengo vya Usimamizi
wa Manunuzi na Idara Nunuzi inayofanyika mjini Dodoma.
Amesema uzoefu
unaonesha kuwa baadhi ya watumishi wa Umma ambao wamepewa dhamana ya kusimamia
michakato ya manunuzi kwenye taasisi zao wamekuwa hatekelezi wajibu wao
ipasavyo na hivyo kusababisha kupatikana kwa wazabuni ambao hawana uwezo wa
kutekeleza kazi husika aau kazi kutekelezwa chini ya kiwango.
Akitolea
mfano baadhi yao, Naibu Waziri Jaffo amesema “baadhi ya wajumbe wa bodi za
zabuni wamekuwa wakishiriki katika vitendo visivyo vya kiuadilifu na mwisho
tunapata wazabuni wasio na vigezo na hivyo kusababisha hasara kwa Serikali”.
Alitoa pia
wito kwa wakuu wa taasisi za umma kuepuka vitendo vya mgongano wa kimaslahi
kwenye michakato ya manunuzi ya umma na kutokubali kuyumbishwa na wasiasa. “Naomba
kuwasihi wakuu wa taasisi msikubali kuyumbishwa na wanasiasa ambao wameingiza
kampuni zao kwenye michakato ya manunuzi kwani hali hiyo husababisha kazi
nyingi kutekelezwa chini ya kiwango na hivyo kukosa thamani ya fedha kwenye
miradi inayotekelezwa kwa fedha za Umma,” alisema Naibu Waziri.
Kwa upande
wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Dkt. Laurent Shirima, alielezea baadhi ya
maeneo yenye changamoto kubwa kwenye manunuzi ya umma kuwa ni pamoja na
usimamizi wa mikataba ya manunuzi. “Eneo la utekelezaji wa mikataba ndilo
linalotumia fedha nyingi kwenye mchakato mzima wa manunuzi ya umma. Hivyo
usimamizi mzuri katika eneo hili ni muhimu sana, lakini tumeshuhudia mapungufu
mengi kwenye eneo hili kupitia ukaguzi ambao ambao tumeufanya katika mwaka wa
fedha 2015/16,” alisema Dkt. Shirima.
Mafunzo hayo
yanayoendeshwa na PPRA ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Katibu Mkuu
Kiongozi, Balozi John Kijazi, ya kuitaka Mamlaka hiyo kuwapatia mafunzo kuhusu
sheria ya manunuzi wakuu wa taasisi za umma ili wawe na uelewa wa kutosha
katika kusimamia shughuli za manunuzi ya umma kwenye taasisi zao.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mheshimiwa Selemani Said Jaffo amewataka watumishi wa Umma wanaoshiriki kwenye michakato ya manunuzi kuzingatia udilifu wakati wanapotekeleza majukumu yao ili kuzuia upotevu wa fedha za serikali zinazoelekezwa kwenye manunuzi mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...