Mhadhama Kardinali Polycarp Pengo na Dkt. Fredrick Kigady wakifuatilia historia fupi ya Tuzo ya BENEMERENTI ambayo upewa mtu aliyetoa mchango wake mkubwa katika kutumikia jamii pamoja na kanisa wakati wa hafla ya kumkabidhi tuzo hiyo Dkt. Kigadya mapema wikiendi hii Jijini Dar es Salaam.   
 
 Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa akizungumza katika hafla fupi ya kumkabidhi tuzo na kumvisha nishani Dkt. Fredrick Kigadye aliyotunukiwa na Baba Mtakatifu Papa. Francis  mapema wikiendi hii. Kushoto ni Mhadhama Kardina Polycarp Pengo, Dkt Fredrick Kigadye na Mkewe.
 Muadhama Kardinali Polycarp Pengo akimkabidhi hati yenye ujumbe maalumu kutoka kwa Baba Mtakatifu Papa. Francis Dkt. Fredrick Kigadye wakati wa hafla ya kumkabidhi tuzo aliyetunukiwa kufuatia mchango wake mkubwa katika kulitumikia Kanisa Katoliki kupitia Idara ya Afya chini ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) mapema wikiendi hii. Kulia ni Mke wa Dkt. Kigadye akishuhudia tukio hilo.
 Muadhama Kardinali Polycarp Pengo akimvisha nishani ya heshima ijulikanyao kwa jina la  Benemerenti (Anayestahili) Dkt. Fredrick Kigadye aliyetunukiwa tuzo hiyo na Baba Mtakatifu Papa Francisco kufuatia mchango wake mkubwa katika kulitumikia Katisa Katoliki kupitia Idara ya Afya chini ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) jana Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mke wa Dkt. Kagadye akishuhudia tukio hilo.
Dkt. Fredrick Kigadye akitoa neno la shukrani kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kwa kutambua mchango wake katika jamii na kanisa kwa ujumla. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...