Mwenyekiti wa UWASMA,Peter Thadeo akiongea na wana Kikundi kuhusiana na swala zima la kujikwamua katika lindi la  umaskini jijini Dar jana.
Katibu mkuu ,Aron Kashaija akiongea na wanakikundi kuhusu maswala mbalimbali yanayoweza kusaidia katika swala zima la kupambana na Umasikini.
Baadhi ya Wanakikundi cha UWASMA Wakiwasikiliza viongozi kujadili maswala mbalimbali ya kimaendeleo jijini Dar es salaam.
Wanakikundi cha UWASMA wakiwa katika picha ya Pamoja


Jamii imetakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano ili kutatua changamoto zinazowazunguka ili kuweza kunyanyuka kiuchumi na kunyanyua pato la Taifa.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa chama cha Umoja wa wanafunzi wa St. Matthew UWASMA,Peter Thadeo na kueleza kuwa changamoto kubwa iliyopo ni suala la umaskini ambalo linapelekea jamii kubwa kutofikia malengo yao na kushindwa kupata mahitaji muhimu.

Thadeo ameongeza kuwa lengo kubwa la kuanzisha chama hicho ni kusaidiana na kunyanyua vipato vyao kupitia uwekezaji kwenye kilimo kwa kuunganisha elimu na nguvu walizonazo.Uwekezaji katika kilimo ni njia bora ya kunyanyua na muhimili mkuu wa kupambana na umaskini.alisema thadeo.

UWASMA ni chama kilichoanzishwa na wanafunzi waliomaliza kidato cha sita katika shule ya sekondari ya st.matthew iliyoko jijini dar es salaam lengo likiwa ni kusaidiana katika masuala mbalimbali ya kiuchumi kwa kupitia uwekezaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...