Na Mwandishi wetu, Dodoma

Kambi Rasmi ya upinzani Bungeni yaikubali Bodi ya Ithibati, Baraza Huru la Habari pamoja na Bima ya Afya kwa waandishi wa habari nchini.

Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni mjini Dodoma, Msemaji Mkuu wa Kambi hiyo katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Joseph Mbilinyi amesema kuwa Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa 2016 unamaufaa kwa wanahabari nchini

“Kifungu cha 58 kinatoa jukumu na kuwataka waajiri wa waandishi wa habarikuhakikisha kuwa waandishi wa habari wanakuwa na bima ya afya pamoja na kuhakikisha kuwa wanachangia katika mifuko ya hifadhi za jamii” alisema Mbilimnyi.Msemaji huyo aliendelea kusema “Jambo hili ni jema sana na Kambi Rasmi ya Upinzani inaliunga mkono”.

Kuanzishwa kwa Bodi ya Ithibati pamoja na Baraza Huru la Habari ni jambo jema vitu ambavyo vitalinda maslahi ya mwandishi wa habari kwa kuzingatia kuwa moja ya kazi Baraza na Bodi ni kuweka viwango vya uangalizi pamoja na utaratibu wa kitaaluma katika kuratibu tasnia ya habari nchini.

Mbilinyi ametoa rai kwa Wabunge wote bila kujali itikadi za vyama kutambua kuwa jukumu la kutunga sheria ni wajibu wao wa kikatiba ambayo wanawajibika wakiwa sehemu ya Bunge kufanya kazi kwa maslahi mapana ya taifa.
 
Msemaji Mkuu wa Kambi Bungeni katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Joseph Mbilinyi akiwasilisha hotuba ya kambi hiyo kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa 2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...