Na Woinde Shizza,Arusha

WASANII mbalimbali jijini hapa wanatarajiwa kuanza kupata neema ya kukuza vipaji vyao baada ya bendi mpya ya muziki kuanzishwa.

Bendi hiyo mpya 'East African ngwasuma music band itakuwa ikifanya kazi zake jijini hapa,ambapo Mkurugenzi wa bendi hiyo ya East African Ngwasuma Music bendi Mukhtar Abdul Bolydo (Obama) alisema ni fursa kwa vijana wenye vipaji vya sanaa ya muziki katika uimbaji kujitokeza ili kuwania nafasi katika bendi hiyo.

"Hivi sasa tumeanzisha bendi hii bado tunauhitaji wa vijana wasiopungua 20 kwani malengo yetu ni kuwa na bendi mbili hapo baadaye na ni wakati wa Arusha kupata burudani ya aina yake",alisema Abdul.

Alisema bendi hiyo itaongozwa na msanii nguli wa muziki kutoka Fm Academia ambaye amehama na kujiunga na bendi hiyo mpya kwa kiasi cha shilingi Milioni 20 na amesaini mkataba wa miaka mitano wa utoaji wa huduma ya muziki.

Msanii huyo 'King of the king'king'(mzee wa mujini) Kingombe Mohammed alisema ataitumikia bandi hiyo kwa ajili ya kutoa burudani."Nimekuwa FM Academia kwa miaka mingi hivi sasa nimehama na tumeamua kuanzisha bendi mpya itakayokuwa moto wa burudani,".alisema Mohammed.

Bendi hiyo mpya ya East African Ngwasuma Music bendi yenye makao yake makuu jijini hapa, ina jumla ya wasanii 12 kati yao wawili wanawake na kila msanii ana mkataba wa miaka miwili na baada ya hapo kama atafanya vizuri ataendelea kutumikia kulingana na uwezo wake.
Picha ikionyesha wa kwanza kushoto mwimbaji wa zamani wa bendi ya FM academia Kingombe Mohamed (kingblez) akisaini mkataba wa miaka mitano wa kufanya kazi katika bendi mpya ya East African Gwasuma music band iliyopo jijini Arusha, anayefuata wa kwanza kulia ni wakili wa bendi hiyo Vivianus Rugakingira,kwanza ni mkurugenzi wa bendi hiyo Muktar Abdu Bolydo (Obama) na wafanyakazi wake wakishuhudia king blez akisaini mkataba wa kufanyakazi katika bendi hiyo kwa miaka mitano .
Mkurugenzi wa bendi hiyo ya East African Ngwasuma Music bendi Mukhtar Abdul Bolydo (Obama) akisaini mkataba wa kumuajiri kingblez kwa muda wa mika mitano ambapo alisema amemchukuwa fm Academia kwa kiasi cha shilingi milioni 20 
 Afisa utamaduni wa jiji la Arusha Benson Maneno akimkabidhi KIng blez mkatabawake mara baada ya kusaini 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...