Habari na Mwene Said wa Blogu ya Jamii, Dar es Salaam.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imesema haimuogopi kumwadhibu Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na  imemuonya tabia yake ya kushindwa kufuata taratibu za kisheria anapokuwa na udhuru siku kesi yake inapopangwa kusikilizwa.

Kadhalika imesema Lissu anatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii, mshtakiwa huyo alishindwa kufika mahakamani mara tatu mfululizo kusikilizwa kesi yake na wenzake watatu dhidi ya mashtaka ya uchochezi kupitia gazeti la Mawio.

Onyo hilo lilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya mahakama yake kutoa amri ya kukamatwa Lissu Novemba 3, mwaka huu.

"Pamoja na nafasi yako uliyonayo kwa jamii lakini ujue kwamba mahakama hatukuogopi labda upande wa Jamhuri ulioshindwa kuja kukukamata ... mahakamani hakuna kuoneana bali taratibu za kisheria zinachukua mkondo wake" alisema Hakimu Simba.

ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya hakimu na Lissu:
Hakimu Simba ; Awali ulikwenda Ujerumani bila kutoa taarifa mahakamani unadhani tunakuogopa?

Lissu; Sina nia mbaya mheshimiwa hakimu nilipelekwa Ujerumani kwa dharula.

Hakimu Simba ; Je, kesi ya Uchaguzi wa Jimbo la Bunda nayo ilikuwa ni dharula?

Lissu; Mheshimiwa hakimu nilipotoka Ujerumani nilikuta kesi ya Bunda imepangwa kusikilizwa na ilikuwa na muda maalumu, niliandika barua Hakimu Mfawidhi wa mahakama hii ya Kisutu na nakala nilielekeza kwa upande wa Jamhuri sina nia ya kuidharau mahakama.
Hakimu; Kutokana na nafasi yako katika jamii ujue kwamba mahakama hatukuogopi labda upande wa Jamhuri ulioshindwa kukukamata na kukuweka chini ya ulinzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...