Mwanzilishi
wa Taasisi ya Her Initiative, Lydia Charles (kushoto) akimtambulisha
Mwenyekiti mpya wa Taasisi hiyo, Irene Enock wakati wa
Kongamano la siku moja lililowajumuisha wanafunzi wakike kutoka vyuo
mbalimbali nchini pamoja na
wadau mbalimbali wanaojishughulisha na biashara, ujasiriamali na vyombo
vya habari, likiwa na lengo la kukuza upeo na uelewa wa wasichana
katika maswala mbalimbali ya maendeleo. Kondamano hilo lilifanyika
mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Yombo 4 ndani ya Chuo Kikuu cha Dar
es salaam.
Her
Initiative iliyojulikana mwanzo kama Teen Girls Supportive Initiative
(TGSI) kwa kushirikiana na DUMA waliandaa Kongamano lililojulikana kama
Panda. Kongamano hilo liliwajumuisha wanafunzi wakike kutoka vyuo
mbalimbali nchini pamoja na wadau mbalimbali wanaojishughulisha na
biashara, ujasiriamali na vyombo vya habari yote katika lengo la kukuza
upeo na uelewa wa wasichana katika maswala mbalimbali ya maendeleo.
Her
Initiative ni asasi ya wasichana ambayo ndio mhimili wa maongezi. Her
Initiative inawapa wasichana nafasi ya kuwakilisha na kusimamia maswala
yao wenyewe ya kiuchumi, elimu, kiutamaduni na kiafya, na inamjengea
uwezo msichana wa kutafuta suluhu ya changamoto zake mwenyewe bila
kutegemea watu wengine. Vyote hivi hufanyika kupitia kampeni, matamasha,
semina na kuwapa msaada wa mahitaji ya kielimu, kiuchumi na kiafya kwa
kushirikiana na wadhamini mbalimbali.
Panda
ni event inayohusu ujasiriamali, uvumbuzi, ubunifu na matumizi mazuri
ya pesa. Kama tunavyofahamu, wasichana tuna matumizi mengi ya pesa na
mara nyingi matumizi haya huzidi kipato cha pesa tunachokipata. Kwa
kuona hilo wasichana hao waliamua kuandaa tamasha ili kusaidiana kuepuka
hatari zinazoweza kutokana na kutokuwa na uchumi imara. Madhumuni ni
kumjengea msichana hali ya kujitegemea kwa kumfundisha namna ya
kuhifadhi pesa kupitia benki tofauti na mifuko mbalimbali ya jamii.
Mkutano
huo uliofanyika katika ukumbi wa Yombo 4 ndani ya Chuo Kikuu cha Dar es
salaam, ulifunguliwa na Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini, Mboni
Mhita ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika shughuli hii. Wageni
wengine waliohudhuria na kutoa maneno ya ushauri kwa wasichana ni pamoja
na Dr. Sebastian Ndege "CEO wa Jembe Group ", Shekha Nasser wa Shear
Illusions, Irene Kiwia mwanzilishi wa Frontline Portel Novelli, Vanessa
Mdee Mwanamuziki,Mc Pilipili Mchekeshaji, Idriss Sultan Mchekeshaji na
Millard Ayo mmiliki wa online Television.
Mbunge
wa Jimbo la Handeni Vijijini, Mboni Mhita ambaye ndiye aliyekuwa mgeni
rasmi katika Kongamano hilo, akitoa nasaha zake kwa wanafunzi
wakike kutoka vyuo mbalimbali nchini katika kukuza upeo na uelewa wa wasichana
katika maswala mbalimbali ya maendeleo.
Mtendaji
Mkuu wa Kampuni ya Jembe Group, Dkt. Sebastian Ndege akitoa mada katika
Kongamano la siku moja lililowajumuisha wanafunzi
wakike kutoka vyuo mbalimbali nchini pamoja na
wadau mbalimbali wanaojishughulisha na biashara, ujasiriamali na vyombo
vya habari, likiwa na lengo la kukuza upeo na uelewa wa wasichana
katika maswala mbalimbali ya maendeleo. Kondamano hilo lilifanyika
mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Yombo 4 ndani ya Chuo Kikuu cha Dar
es salaam.
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Shear Illusions, Shekha Nasser akitoa mada katika Kongamano la siku moja lililowajumuisha wanafunzi wakike kutoka vyuo mbalimbali nchini pamoja na
wadau mbalimbali wanaojishughulisha na biashara, ujasiriamali na vyombo
vya habari, likiwa na lengo la kukuza upeo na uelewa wa wasichana
katika maswala mbalimbali ya maendeleo. Kondamano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Yombo 4 ndani ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...