Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji ,Clifford Tandari akizungumza na baadhi ya Watumishi wa Kituo hicho pamoja na Waandishi wa Habari wakati walipotembelewa na balozi wa Israel kuzungumzia Kongamano la Biashara na Uwekezaji litakalofanyika Tel Aviv Israel. 
Balozi wa Israel Nchini Tanzania,Yahel Vilan akizungumzia Kongamano hilo ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika nchini Israel baada ya kufanyika Tanzania kwa mara ya Tatu mfululizo.
KITUO  cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya nchi za nje na Taasisi za Sekta binafsi Tanzania  kimeandaa kongamano maalum  la kuamasisha na kukuza uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Israel kwa lengo la kuisaidia na kuitangaza tanzania kama ni miongoni mwa maeneo yenye fursa na mazingira mazuri ya kibiashara kwa kampuni  nyingi za Israeli.

Kongamano hilo ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika nchini Israel  baada ya kufanyika Tanzania mara tatu mfulilizo  linatarajia kufanyika kuanzia tarehe 28 novemba hadi 30 mwaka huu ambalo litahudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wawekezaji, wafanyabiashara wakubwa na wataalamu mbalimbali huko Tel Aviv Isrel.

Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji , Clifford Tandari amesema kuwa malengo ya Kongamano hilo ni kutoa fursa za biashara na uwekezaji zilizopo hapa nchini kwa wawekezaji wa Isrel ambazo zipo maeneo katika sekta mbalimbali kama vile viwanda, kilimo na Usindikaji wa mazao,Nishati, Afya,Teknologia, Elimu, Maji ,Majengo,Chakula ,Dawa, Utafiti na Maendeleo.

Bw.Tanadri ametoa two kwa makampuni ya Tanzanania kwenda kushiriki  kongamano hilo ili kuanzisha na kukuza ushirikiano katika nyanja za biashara na uwekezaji kwa kushirikiana na Kampuni na wafanyabiashara wa Israel, kwani kuna uwezekano mkubwa  Tanzania ikaongeza thamani yake.thamani ya mitaji na uwekezaji  kutoka nje iwapo makampuni ya Israel yatakayohudhuria kongamano hilo yataamua kufanya uwekezaji.

"Tunatoa wito kwa makampuni yetu ya Kitanzania yaweze kwenda kushiriki katika kongamano hili maana ni fursa za kipekee sana,” amesema Tandari

Naye Mh.Balozi wa Israel Nchini Tanzania Bw.Yahel Vilan ameeleza kuwa amefurahishwa na  kongamano hilo na anaamini kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zitashiriki vizuri Kongamano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...