Meya
Mstaafu wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda ameitaka jamii kuunga
mkono juhudi za Rais John Magufuli za kuboresha Sekta ya elimu kwa
kuchangia maendeleo ya elimu ili kuleta mabadiliko ya elimu nchini.
Meya
huyo Mstaafu ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Maabara ya kisasa ya
kompyuta ya Shule ya Sekondari Mikocheni, Dar es Salaam kwa udhamini wa
kampuni ya intaneti ya Raha Broadband kwa kushirikiana na yeye mwenyewe
hivi karibuni.
Hiyo inakuwa ni miongoni mwa Maabara chache bora za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano nchini kwa shule za Umma.
Mwenda
aliutaka uongozi wa shule hiyo kuitunza maabara hiyo na kuitumia vizuri
ili faida yake ionekane kwenye matokeo ya mitihani ya shule hiyo.
"Tukubaliane
kuwa mtaitunza maabara hii vizuri ili umuhimu wake uonekane katika
matokeo ya mitihani ya wanafunzi". Alisema Mwenda.
Aidha
aliishukuru kampuni ya Raha Broadband kwa kuchangia kompyuta na vifaa
pamoja na huduma ya intaneti kwa kila mwezi vyenye thamani ya shilingi
milioni 18 na kuwataka viongozi wa Manispaa hiyo kuwashawishi wananchi
nao kuchangia maendeleo ya elimu kwa shule za Manispaa hiyo.
Kwa
upande wake Meya huyo Mstaafu alichangia shilingi milioni 3.9 ikiwa ni
ukarabati wa Chumba cha maabara, madirisha, milango pamoja na meza za
kompyuta.
Naye
Meya mpya wa Manispaa hiyo, Benjamin Sitta alimshukuru Meya huyo
Mstaafu pamoja na kampuni ya Raha kwa mchango wao na kuomba waendelee
kumsaidia kwa shule nyingine za Manispaa hiyo.
Meya
Mstaafu wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda (kushoto), Meya mpya wa
Manispaa hiyo, Benjamin Sitta (wa pili kulia), Ofisa Mtendaji Mkuu wa
Kampuni ya Raha Broadband, Aashiq Shariff (wa pili kushoto) na Diwani wa
Kata ya Mikocheni, Bethel Kimei (Mama Langa).
Meya
wa Manispaa ya Kinondoni Benjamin Sitta na Meya Mstaafu wa Manispaa
hiyo, Yusuf Mwenda (kushoto) wakimtazama mwanafunzi wa Shule ya
Sekondari Mikocheni, Jamila Msami akitumia kompyuta baada ya ufunguzi
rasmi wa Maabara ya kisasa ya kompyuta ya shule hiyo kwa ufadhili wa
Kampuni ya intaneti ya Raha Broadband, Dar es Salaam juzi.
Meya
Mstaafu wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda akizungumza wakati wa
ufunguzi wa Maabara ya kisasa ya kompyuta ya Shule ya Sekondari
Mikocheni, Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni
ya intaneti ya Raha Broadband, Aashiq Shariff na Meya mpya wa Manispaa
hiyo, Benjamin Sitta.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...