Maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani, ambayo kitaifa yalitarajiwa kufanyika jijini Dar es salaam,Desemba 3, mwaka huu yameahirishwa na badala yake kila mkoa utaadhimisha kivyake.

Akitoa tamko la kuharishwa kwa maadhimisho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), George Simbachawene amesema maadhimisho hayo yalilenga kila halmashauri isafirishe wanachama wa vyama vya watu wenye ulemavu ili washiriki maadhimisho hayo jijini humo.

Amesema kwa mujibu wa maelekezo aliyopewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa wakuu wa mikoa kuwa badala ya maadhimisho hayo ya kitaifa kukusanya walemavu wote kwenye mikoa kwenda Dar es salaam yafanyike kwenye mikoa yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...