Mkuu wa Kitengo cha upasuaji wa Kifua na Moyo BMC, Prof. William Mahalu akizungumza (kulia) kwenye mkutano na waandishi wa habari wakati wa kuwakaribisha madaktari bingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai, India katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza, pembeni yake ni Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani.
 Gharama za upasuaji wa Moyo ni kubwa si chini ya shilingi Millioni 6 za Tanzania. Kwa wagonjwa hawa tunashukuru Wizara ya Afya,Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Medical Centre (BMC) lakini shukurani nyingi ziende MMI ambao wamenunua vifaa vingi ba ambavyo watatuachia hapa, ili tuendelee naupasuaji huu.
Sehemu ya madaktari wageni toka nchini India wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari wakati wa kuwakaribisha madaktari hao mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai, India katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza. Wa pili kutoka kushoto ni Bingwa wa Moyo kwa watoto daktari mzalendo aliyerejea nchini Dr. Glory Joseph ambaye ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi hilo. 

Kwa mujibu wa Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani (katikati) amesema kuwa kila mwaka Hospitali ya Aga Khan inatumia shilingi za Kitanzania bilioni 2 kuwahudumia wagonjwa bila malipo yoyote ambapo hadi sasa zaidi ya wagonjwa 600 wamefanyiwa upasuaji wa moyo.
Watanzania madaktari 10 walipelekwa nchi za nje kupata mafunzo zaidi. Aidha Wakfu wa Afya wa Aga Khan umewekeza shilingi za kitanzania bilioni 167 katika ujenzi wa Hospitali ya kisasa ya kutoa mafunzo ya udaktari ambayo tayari imeanza kujengwa. 
Pia kujengwa vituo 35 vya afya vitajengwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini, vitano vikiwa katika mkoa wa Mwanza. Kupata zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...