Benjamin Sawe-MAELEZO

Katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano kumefanyika jitahada kubwa za kuhakikisha inafufua mashirika yalifikia hali mbaya na kushindwa kutoa huduma ili hatimaye yaanze upya kutoa mchango wa ujenzi wa uchumi nchi. Mojawapo wa Mashirika hayo ni pamoja na Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ambapo kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani lilikuwa na Ndege mmoja tu.

Hatua hiyo ya Rais Magufuli kuamua kununua Ndege mbili aina ya Bombadier Q400 zimesaidia kuimarisha Kampuni hiyo na kurejesha nembo ya Twiga iliyoanza kupotea. Licha ya juhudi hizo na kazi mkubwa aliyoifanya Rais Magufuli ya kutimiza ahadi yake ya kuanza kuijenga upya Kampuni hiyo, wapo baadhi ya wananchi wachache ambavyo wamewakuwa hawana shukurani na kuanza kubeza jitihada hizo.

Ni vema wakumbe ule usemi unaotumiwa na baadhi ya watu kuwa “ Hata mbuyu ulianza kama mchicha” .Kauli hii inadhihirisha kuwa kila jambo uwa na mwanzo wake kwani tokana na dhihaka za baadhi ya watu ambao wamekuwa wakibeza juhudi za Mhe. Rais Magufuli. Ununuzi wa Ndege hizo umesaidia kumeimarisha huduma za usafiri wa anga na kuongeza ushindani katika utoaji wa huduma za anga hapa nchini kati yake na kampuni binafsi za ndege zinazotoa huduma hiyo kwa sasa

Azma hiyo ya Serikali ya kununua ndege mpya imetimiza ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli wa kulifufua tena Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na kulipatia mtaji ili lianze upya kutoa huduma hiyo kwa Watanzania. Akizindua ndege hizo Rais Magufuli alisema kuwa ,ndege hizo zina sifa ya matumizi madogo ya mafuta na ni suluhisho la kupanda kwa bei ya usafiri wa anga nchini na pia zitasaidia kukuza sekta ya utalii nchini.

“Ndege hizi zinatumia wastani wa mafuta ya shilingi milioni moja kutoka hapa hadi Songea, wakati ndege za Jet zinatumia mafuta ya shilingi milioni 28.1 kwa safari kama hiyo,” anasema Mheshimiwa Rais. Ukitaka kujenga nchi yenye uchumi wa kisasa huwezi kujenga bila kuwa na ndege na ukitaka watalii lazima uwe na ndege.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...