Na Walter Mguluchuma wa Katavi yetu Blog
Hifadhi ya Taifa ya Katavi inapatikana kusini Magharibi mwa Tanzania karibu na Ziwa Tanganyika katika Wilaya za Mpanda ,Tanganyika na Mlele Mkoa wa Katavi inapatikana katika latitude 6.63.7.34 kusini na na longitude 3.74.31.84 Mashariki.
Hifadhi hii ilitangazwa kuwa Hifadhi ya Taifa mwaka 1974 ikiwa na ukubwa wa kilometa za mraba 2253 iliongezwa ukubwa mwaka 1996 na kufikia ukubwa wa kilometa za mraba 4471 na kuifanya kuwa Hifadhi ya tatu kwa ukubwa Tanzania baada ya Ruaha na Serengeti .
Ilipata jina lake kutokana na mzimu wa kabila la Wabende aliyejulikana kwa jina la Katabi ambapo mpaka leo watu mbalimbali wamekuwa wakifika ndani ya Hifadhi ya Katavi na kwenda kwenye mti ulioko kwenye Ziwa Katavi wakiamini kuwa mzimu Katabi alikuwa akiishi hapo zamani kabla ya kuwepo Hifadhi ya Taifa ya Katavi .
Jina la Hifadhi hii lilijulikana kama Katabi kutokana na imani ya jamii hizo kwa mzimu Katabi inaaminika kwamba mzimu Katabi una uwezo wa kufanya miujiza ikiwemo kufanya mvua inyeshe , kuzuia magonjwa ya mlipuko kama vile ndui na kutatua shida za watu mbalimbali .
Hawa ni Punda milia wakiwa katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi
Kama kibao kinavyo onekana hili ni Eneo la Tambiko ambapo watu huja kusali na kutoa sadaka mbalimbali
Simba akiwa na mzoga wa Kiboko
Twiga akiwa katika hifadhi ya Taifa ya Katavi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...