MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda, amefanya ziara kwenye Makao Makuu ya klabu ya Azam akiwa na lengo kuu la kuipongeza kutokana na juhudi kubwa wanazofanya za kuwekeza katika kukuza vipaji vya vijana na kutoa wito kwa watu wengine wenye uwezo kujitokeza, na kuiga mfano wa Azam ili kuwa na timu nyingi zenye ushindani na kuondoa migogoro kwenye soka la Tanzania.

Kwenye msafara huo, Makonda aliambatana baadhi ya viongozi wengine wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, alikofanya ziara tofauti kusikiliza kero za wananchi wa wilaya hiyo akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya hiyo, Felix Jackson Lyanivana na ugeni huo ulipokelewa na viongozi wa juu wa Azam FC, wakiongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu, Saad Kawemba, Makamu Mwenyekiti, Nassor Idrissa, Meneja wa timu, Phillip Alando, ambao katika kumalizia ziara hiyo waliweza kumtembeza kwenye maeneo mbalimbali yaliyofanyiwa uwekezaji ndani ya Azam Complex oliyopo Chamazi.

Akitoa neno lake kwenye ziara hiyo, Makonda alisema haina ubishi kuwa Azam ndiyo timu pekee iliyofanikiwa kuwekeza ipasavyo kwenye soka huku akidai kuwa timu hiyo imeshaanza kwa vitendo kutekeleza suala la kupunguza idadi ya vijana walioko mtaani wasiokuwa na dira wala matumaini, “Leo hii mnatuunga mkono zaidi kwa sababu ni kiwanja kimoja na ni timu moja ambayo kila mtu aliye kwenye mkoa wa Dar es Salaam anaizungumzia, katika suala zima la kupunguza idadi ya vijana walioko mtaani wasiokuwa na dira wala matumaini nyinyi Azam mmeshaanza kutekeleza kwa vitendo na watu wote hatuwezi kuajiriwa serikalini, haiwezekani leo serikali ikaajiri watu wote.

Watu wengine waige mfano wa Azam, watengeneze timu zao, watengeneze viwanja ili tuwe na watu wengi, tuwe na timu nyingi zenye ushindani na hata hii migogoro inayotokea Yanga na Simba, wenye hela zao wasihangaike kama wamegoma kukodishwa wafanye maamuzi ya kutengeneza timu zao ili na wenyewe waendelee kunufaika kwa sababu mwisho wa siku tunajua tukiwa na timu nyingi kama ilivyo Azam ushindani utakuwa mkubwa sana.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda akionyesha jezi ya Azam aliyokabidhiwa na Ofisa Habari wa Azam Fc Jaffar Iddy wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye Makao Makuu ya Klabu hiyo leo Jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda(wa kwanza kushoto) akiongea na baadhi ya watendaji wa klabu ya Azam Fc wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye Makao Makuu ya Klabu hiyo leo Jijini Dar es salaam.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (aliyesimama) akizungumza kwa niaba ya uongozi wa Azam FC na kumshukuru Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda kwa ugeni wake huo wenye tija kwao.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda akiwa anatembelea maeneo mbalimbali ya Uwanja wa Azamuliopo Chamazi baada ya kufanya ziara leo Jijini Dar es salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...