Mtu mmoja aliye fahamika kwa jina moja la Mwita na mfanyabiashara wa nyama ya ng'ombe afanyae bishara zake eneo la Mwanjelwa, amekutwa amefariki dunia asubuhi hii katika eneo la Mafiati jijini Mbeya akiwa ametokwa na damu nyingi kichwani ikisemekana kuwa "alivamiwa na kupigwa na watu wasio julikana". Pichani Mwili wa marehemu Mwita ukiingizwa kwenye Gari ya Polisi.
Huzuni ikiwa imetawala kwa ndugu jamaa na marafiki eneo hilo la tukio huku wakipeana taarifa kuwajuza wengineo juu ya tyukio hilo lililo Tokea asubuhi hii eneo la Mafiati Jijini Mbeya.
Jeshi la Poli likiondoka na mwili wa marehemu
PICHA NA MR.PENGO WA MMG.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...