Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na  Uwekezaji, Charles Mwijage amesema Tanzania imeweka mazingira bora ya uwekezaji wa biashara kupitia Kituo cha Uwekezaji  Nchini (TIC).

Akizungumza katika Mkutano kati wa Wafanyabiashara wa Tanzania na  Ubelgiji, Mwijage amesema kuwa mazingira yaliyowekwa ni rafiki kwa uwekezaji katika mbalimbali ikiwemo ya Kilimo  cha biashara.

Mwijage amesema kuwa Tanzania ni nchi inayokua kwa kasi duniani hivyo wawekezaji wana nafasi ya kufanya uwekezaji kutokana na kuwa nchi ya amani ambapo wawekezaji wanaweza kuwekeza na kuzalisha bila kuwepo kwa vikwazo.

Amesema kuwa serikal ya awamu ya tano inapambana na rushwa ili kuweza wananchi waweze kuishi bila rushwa.

Mwijage amesema maeneo ya kufanya uwekezaji yamepanagwa katika maeneo ya biashara, kilimo, Miundombinu, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Madini,  Gesi , Utalii pamoja Uvuvi.

Amesema kuna ushirikiano wa muda mrefu kati Tanzania na Belgium hivyo milango ya uwekezaji iko wazi na nchi nyingine zimeweka mikakati ya uwekezaji.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charle’s Mwijage akizungumza na wafanyabiashara wa nchi ya Ubelgiji juu ya serikali ya Tanzania kuweka wazi milango ya uwekezaji leo jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Kundi la Wafanyabiashara wa Umoja wa Ulaya, Rose Blackie akizungumza katika mkutano wa wafanyabishara uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC, Clifford Tandari akizungumza na wafanyabiashara wa nchi ya Ubelgiji juu ya serikali ya Tanzania kuweka wazi milango ya uwekezaji leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Wafanyabiashara wakiwa katika Mkutano wa kuangalia juu ya uwekezaji leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...