Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh
Richard Kasesela amezindua mradi wa maji katika kijiji cha Lupalama kilichopo
katika Tarafa ya kalenga Wilayani Iringa uliodhaminiwa na Shirika la
E.P.I.C (Everyday People Initiate Changes) la Marekani liloanzishwa na
Mwanamuziki wa Marekani Tinara Moore. ambaye aliwahi kutembelea Tanzania na
baadae kuamua kutoa misaada mbalimbali.
Wanakijiji wa Lupalama kwa muda
mrefu wamekuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta maji, “Tulikuwa tukilazimika
kutembea saa zima kufata maji mtoni nabado maji haya kuwa ya uhakika kwa maana
kipindi cha kiangazi mto ulikuwa una kauka jambo lililopelekea kupata shida
kubwa sana katika upatikanaji wa maji” anaeleza
Bi Theobadina Ngailo mkazi wa Lupalama anaongeza kuwa “Tulikuwa tunatumia hata
maji ya kwenye vidimbwi ambayo sio salama kwa matumizi ya binadamu kwani muda
mungine tulikuwa tukichangia maji hayo na mifugo jambo lilipolekea kulipuka kwa
magonjwa kama kuhara”.
Akizungumza wakati wa kukabidhi
mradi huo Muwakilishi wa E.P.I.C Tanzania Bwana Johnson Mkini Kisinda amsema
kuwa mradi huo umeghalimu pesa zaidi ya milioni therasini na tano hadi
kukamilika “Hiki ni kisima cha pili kwa urefu katika visima vyote tulivyo
chimba kwani Lengo lilikuwa kuchimba mita sabini tu ila tulikosa maji
tukalazimika kuchimba mita mia moja na themanini kwenda chini hadi kuyafikia
maji”, pia ame waasa wanakijiji wa Lupalama kuwa walinzi wa miundo mbinu hiyo
ya maji kwani ni kwa faida yao wenyewe.
Akikabidhi Mradi huo kwa
wanakijiji wa lupalama mkuu wa wilaya ya Iringa amewaomba wana kijiji hao kuusimamia vema mradi huo
kwani Ofisi yake ina mpango wa kuhakikisha maji hayo yana sambazwa katika
Maeneo Yote ya kijiji hicho ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa wingi “Ni
ndoto yangu kuona Maji haya yana wafikia wanakijiji wote wa lupalama ikibidi na
maeneo ya Jirani wapate pia maji haya nitoe agizo kwa serikali ya kijiji kuunda
kamati ya kusimamia na kutunza mradi huu ili uendelee kufanya kazi na
kunufaisha wengi wakati mimi niki hangaika kuona jinsi gani tunapata pampu ya
Umeme ikishindikana hata ya kutumia nguvu ya jua ili tusambaze maji haya sehemu
nyingi zaidi”.
Pia ameagiza Serikali ya kijiji
Kuanza mara moja Mchakato wa ujenzi wa kituo cha afya kijijini hapo kwani ni
kero ya muda mrefu hasa kwa akina mama kwani wana lazimika kutembea kilomita
saba kufuata huduma ya afya “Nawaombeni Zoezi hili lianze mapema sana na ikibidi kila mwanakijiji
ashiriki kukusanya mawe ya ujenzi na pindi mkiwa tayali ujenzi uanze mara moja”.
Katika hotuba yake Mkuu wa wilaya
pia amehimiza watu kutunza chakula “ mvua mwaka huu sio za kuridhisha hivyo
basi ipo hofu ya kukosekana chakula ni muhimu wananchi wakatunza chakula na
kulima mazao yenye kuhimili ukame”
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela akikata utepe kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Lupalama kilichopo katika Tarafa ya Kalenga Wilayani Iringa. Kulia kwake ni bwana
Johnson Kisinda muwakilishi wa E.P.I.C Tanzania Kushoto ni Diwania wa Lupalama.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela akichota maji baada ya kuzindua mradi huo katika kijiji cha Lupalama kilichopo katika Tarafa ya Kalenga Wilayani Iringa
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela akimtiwka Bi. Theobadina Sengailo ndoo ya maji baada ya kuzindua mradi huo katika kijiji cha Lupalama kilichopo katika Tarafa ya Kalenga Wilayani Iringa
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela katika hafla ya kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Lupalama kilichopo katika Tarafa ya Kalenga Wilayani Iringa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...