Na Mwandishi Wetu
Kambi tiba ya GSM Foundation, mpaka jana jioni ilikuwa
imefikia mikoa 18 ya Tanzania Bara na mmoja wa Tanzania Visiwani ambapo
kwa ujumla wake, imefanikiwa kuwaona watoto zaidi ya 3000 na kuwafanyia
oparesheni zaidi ya watoto 250.
Kaimu
Mkurugenzi wa taasisi ya Mifupa, Upasuaji na Mishipa ya Fahamu ya
Muhimbili, Dk Othman Kiloloma ambaye pia ndio kuwa Kambi tiba hiyo ya
GSM Foundation, amesemahata hivyo wako katika kujipanga na kuona iwapo
wanaweza kurudia mikoa ya Rukwa na Pemba ambao kuna uhitaji.
Jana
wanakambi wa GSM walimaliza kazi yao visiwani Unguja ambayo kwa mujibu
wa Afisa Habari wa GSM Bw Khalfan Kiwamba ilikuwa ni Awamu ya tano ya
kambi tiba hiyo na kurudi Dar kufanya tathmini ya kazi iliyofanyika, na
kujua jinsi ya kumaliza kabisa tatizola watoto wanaozaliwa na vichwa
vikubwa na mgongo wazi.
Dkt.
Yassin Juma kutoka Kitengo cha MOI akiwa katika maandalizi ya kumfanyia
upasuaji wa kichwa mmoja ya watoto waliofika Hospitali ya Mnazi mmoja
kufanyiwa tiba hiyo.
Dk
Kiloloma alisema kuwa utafiti uliofanywa na Taasisi ya MOI mwaka 2002
unaonyesha zaidi ya watoto 4800 huzaliwa kila mwaka wakiwa na maradhi ya
vichwa vikubwa na migongo wazi na kati yao 500 pekee ndiyo wanaoweza
kufika hospital na kupatiwa matibabu.
Akizungumzia
chimbuko la maradhi hayo Dk Kiloloma alisema kuwa watoto wenye vichwa
vikubwa na migongo wazi wanaweza kuzaliwa nacho au kupata siku chache
baada ya kuzaliwa.
"Kwa
wale wanao zaliwa na maradhi hayo ni kwa sababu ya upungufu wa
virutubisho ambavyo mama mjamzito anatakiwa avipate kabla ya kushika
mimba virutubisho hivo vinapatikana kwenye matunda,mboga za majani,mayai
na vyakula vyote vyenye protini, pia maradhi ya mgongo wazi husababisha
watoto kupooza na kushindwa kutumia miguu yao,"alisema
Daktari
bingwa wa upasuaji wa ubongo na mishipa ya fahamu ambae pia ni Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya MOI Othman Kiloloma akimueleza Waziri wa
Afya Zanzibar (hayupo pichani) jinsi Taasisi hiyo inavyookoa maisha ya
watoto wanaokabiliwa na maradhi hayo, (kulia) ni Afisa Habari wa GSM
Foundation Khalfani Kiwamba.
Ofisa
habari wa GSM Foundation Khalfani Kiwamba alisema kuwa taasisi yao
iliamua kudhamini matibabu ya maradhi ya vichwa vikubwa na migongo wazi
baada ya kuelezwa changamoto mbalimbali za matibabu ya maradhi hayo na
uongozi wa Taasisi ya MOI.
Joviti
Mchuruza akiongea kwa niaba ya wazazi ambao watoto wao wamefanyiwa
upasuaji aliwashukuru timu nzima ya madaktari hao pamoja na Taasisi ya
GSM kwa msaada huo wa matibabu waliowapatia wa watoto wao bure. Aliiomba
jamii kuacha kuhusisha maradhi hayo na mila potofu za imani za
kishirikina au mikosi kwenye familia hali inayofanya akina mama au baba
kutelekezewa watoto.
Waziri
wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na ujumbe wa Taasisi ya MOI na
GSM Foundation ambao wapo Zanzibar kuwafanyia upasuaji watoto wenye
vichwa vikubwa katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...