Mgahawa mkubwa unaotoa huduma za
chakula cha Kitanzania unaomilikiwa na mpishi maarufu duniani, Issa
Kapande `Chef Issa', umefunguliwa nchini Sweden na kuvunja rekodi ya
dunia.Mgahawa huo ulizinduliwa na balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu.
Balozi
Msechu alimpongeza Issa Kapande na mkewe kwa kufanikisha kuwapo kwa
mgahawa huo ambao umeweka rekodi kuwa mgahawa mkubwa kuliko yote ya
Kiafrika katika nchi za Ulaya.
Aidha, alimshukuru Torvald Brahm
mwenyeji wa mji huo kwa kumuunga mkono Issa hadi kufanikisha ndoto yake
ya kuwa na mgahawa wa kwanza wa Kiafrika katika mji wa Trollhattan
utakatoa huduma ya chakula cha kitanzania.
Katika uzinduzi huo
ambapo wenyeji wa manispaa hiyo akiwemo Meya na mwenyekiti wa
Trollhattan, Paul Akerlund na msaidizi wake Peter Eriksson walikuwepo,
balozi ambaye ndio kwanza ameanza kazi alielezea kufurahishwa na juhudi
za Kapande.
Alisema Issa ameonesha njia kwamba inawezekana kwa
watu waliopo Ughaibuni sio tu kuajiriwa, bali kujiajiri katika nyanja
mbalimbali.Alisema hilo linawezekana kutokana na kufuatilia kwa karibu
taratibu za wenyeji na kisha kutumia mafunzo yaliyopo kukamilisha
ndoto."Ni dhahiri kuwa, Chef Issa kwa kupitia taaluma yake ya
upishi amewezeshwa kumiliki mgahawa huu hapa Trollhattan,S weden kwa
hilo, napenda tuishangilie na kuipigia makofi Sweden na
Trollhattan."Alisema akimpongeza kijana huyo ambaye pia amewekeza mkoani
Mtwara.
KUSOMA ZAIDI KWA CHANZO;BBC
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...