Na Anthony John blog Jamii.

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii limekamilisha mradi wa Jengo refu Afrika Mashariki-Mzizima Tower lililopo barabara ya  Azikiwe na Mkwepu Dar es salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Makao Makuu ya Shirika hilo,Mkurugenzi wa Shirika hilo Prof. Godius Kahyarara  amesema Jengo hilo lipo hatua za mwisho za ukamilishaji wa ujenzi ambalo litakuwa na ghorofa 30 za makazi na 32 za Biashara.

Pia amesema Jengo hilo litakuwa na hoteli ya Nyota 5 na nyumba za makazi kwa ajili ya kuuza na kupangisha,Jengo linatarajiwa kukamilika mwakani 2017.Aidha Shilika hilo limesaini makubaliano na atakayekuwa muendeshaji wa Hoteli hiyo itakayokuwa katika Jengo la Mzizima na kutarajiwa kuanza kazi Mara moja baada ya Hoteli hiyo kufunguliwa.

"Baadhi ya miladi imekamilika na mengine ipo katika hatua za ukamilishwaji,NSSF inafungua rasmii upangishwaji wa litakalo kuwa Jengo refu Afrika Mashariki Mzizima Touwers" hayo amesema Kahyarara.
Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF,Prof. Godius Kahyarara akizungumza na Waandishi kuhusiana na mradi wa Jengo la NSSF (Mzizima Tower) .

Baadhi ya Watumishi wa Shirika hilo wakiwa katika picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...