Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma.

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeishauri Serikali kuanzisha mfumo maalum wa uwekezaji ili fedha zitakazowekwa katika mfuko huo zitumike kama mtaji katika maeneo ambayo nchi inataka kuwekeza.

Ushauri huo umetolewa mjini Dodoma na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka alipokuwa akiwasilisha maoni ya kamati hiyo iliyochambuliwa kwa kina juu ya changamoto, maombi na mapendekezo yatakayoiwezesha nchi kusonga mbele.

Mwenyekiti Mhe. Kaboyoka amesema kuwa ushauri huo umetolewa baada ya kukwama kwa baadhi ya miradi pamoja na shughuli nyingine za Serikali zinazofanywa ili kuwasaidia wananchi kutokana na ukosefu wa fedha za kufanyia shughuli hizo hivyo kuanzishwa kwa mfuko huo kutahakikisha faida ya uwekezaji inaonekana.

“Sisi kama kamati tunaishauri Serikali kuanzisha mfuko maalum wa uwekezaji kwani utaisaidia Serikali kupata fedha za kufanyia maendeleo na kupata mitaji ya kuwekeza sehemu mbalimbali ili kuhakikisha maslahi ya nchi yanalindwa na watanzania wanaiona faida ya uwekezaji”, alisema Mhe. Kaboyoka.

Mhe. Kaboyoka aliongeza kuwa kamati hiyo imependekeza kuwa mfuko huo uanzishwe chini ya Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kutumia mfumo wa kubakisha mapato kwa sababu ofisi hiyo ndiyo ina mamlaka ya kugawa fedha za Serikali kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...