Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Shirika la Plan International limezindua Mradi wa Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia ya Michezo ili kuwajengea uwezo wa kuwa mawakala hai wa mabadiliko chanya katika jamii zinazowazunguka.

Mradi huo umezinduliwa leo Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo, Wanchoko Chinchibera ambaye ametoa wito kwa watendaji wa Serikali, wazazi pamoja na jamii kwa ujumla kutoa ushirikiano wa hali ya juu ili kuhakikisha mradi huo unatekelezeka.

Chinchibera amesema mradi huo umekuja wakati muafaka kwani watoto na vijana wanakabiliwa na changamoto ya ulinzi, usawa wa kijinsia pamoja na ushirikishwaji mdogo katika michezo hivyo kupitia mradi huo watapata maendeleo mazuri ya kielimu na kimakuzi pamoja na fursa ya kutatua changamoto zao. 

“Kupitia michezo tunajenga afya, akili, malezi na makuzi ya mtoto lakini pia michezo ni sehemu ambayo watoto wanaweza kupaza sauti zao na kujadili kuhusu haki zao za msingi kwa njia ya nyimbo na mashairi hivyo tunaamini kuwa tukianza kuwashirikisha watoto katika suala zima la michezo tutatengeneza kizazi chenye maendeleo,”alisema Chinchibera.
 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Kisarawe, Mkoani Pwani, Wanchoko Chinchibera akiongea na wanafunzi pamoja na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia ya Michezo uliozinduliwa leo wilayani humo.Mradi huo unaratibiwa na Shirika la Plan International.
 Meneja Miradi wa Shirika la Plan International, Grace Semwaiko akielezea kuhusu malengo ya mradi wa Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia ya Michezo uliozinduliwa leo wilayani Kisarawe.Mradi huo unaratibiwa na Shirika la Plan International.


Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Kisarawe, Mkoani Pwani, Wanchoko Chinchibera akikagua timu ya mpira ya watoto wakati wa mradi wa Kuwawezesha Vijana na Watoto kwa Njia ya Michezo uliozinduliwa leo wilayani humo.Mradi huo unaratibiwa na Shirika la Plan International.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...