Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa kimataifa wa Usafirishaji Duniani utakaofanyika katika mji wa Ashgabat nchini Turkemistan kuanzia tarehe 26-27 Novemba, 2016.

Ajenda kuu ya mkutano huo ulioitishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambao utashirikisha viongozi mbalimbali utajadili kwa kina maeneo muhimu ya ushirikiano wa kimataifa kwenye Sekta ya Usafirishaji kwa maendeleo endelevu Duniani.

Aidha katika mkutano huo Waziri Prof. Mbarawa atapata fursa ya kukutana na wawekezaji mbalimbali Duniani waliobobea katika sekta ya usafirishaji na kuwashawishi kuwekeza hapa nchini.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...