Kampuni inayotoa huduma ya usafirishaji wa anga hapa nchini Qatar Airways kwa miongo kadhaa sasa, kupitia safari zake za Dar es Salaam, Kirimanjaro na Zanzibar imechangia madawai 100 katika shule ya msingi Chanzige B, iliyopo wilayani Kisarawe jijini Dar es Salaaam. Hiyo ikiwa ni sehemu ya mradi wa kusaidia juhudi za serikari kupitia mpango wa kuondoa uhaba wa madawati nchini kwa shule za Msingi pamoja na Sekondari, lakini pia wakiwa kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii.

Makabidhianao hayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya Chanzibe B,ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali, akiwemo Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo, Meneja wa Qatar Airways Tanzania, Basel Haydar, pamoja na wafanyakazi wa Qatar Airways na wawakilishi kutoka ofisi ya Doha pamoja na Daktari Amon Mkoga, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Amon Mkoga Foundation, Bodi ya wakurugenzi na walimu wa shule ya msingi Chanzige B.
Wakati wakikabidhi mchango huo wa madawati, Meneja wa Qatar Airways Tanzania Basel Haydar, amemueleza Naibu Waziri kuwa Qatar Airways itaendelea na mpango wa kusaidia jamii kwa kushirikiana na Serikali katika kuinua na kuimarisha sekta ya elimu nchini.

Akiongea baada ya kupokea madawati hayo, Naibu Waziri Jafo ameipongeza kampuni ya Qatar Airways kwa msaada wanaouonyesha, “Nawapongeza Qatar Airways kwa msaada huu, hii inaonyesha wazi kuwa ni jinsi gani wanavyothamini elimu ya watoto wetu na mazingira kwa ujumla, ambayo yanajumuisha madawati haya waliyokabidhi.

Elimu nzuri ndiyo itakayopeleka kizazi chetu katika uzalishaji mkubwa na kukuza uchumi wa nchi yetu”

 Mwalimu Mkuu wa Chanzige B, Pius Karinga, ametoa shukurani kwa kusema kuwa “Tunaamini maboresho ya shule na mazingira ya kazi kwa Walimu nchini ni chachu ya kuongeza ufanisi wa kuimarika kwa Mwanafunzi ambaye atakuwa na uwezo imara na kuwa sehemu ya uzalishaji muhimu wa rasilimari watu nchini, hivyo basi tunatoa shukrani zetu zadhati kwa Qatar Airways kwa mpango wao wa kuboresha mazingira yetu”.

Qatar Airways ilichagua kushirikana na Daktari Amon Mkonga Foundation katika kusaidia sekta ya elimu nchini kwa kuwa wafanyakazi na sekta zingine mbalimbali wamepatikana kutokana na mazingira mazuri ya kujifunzia. Hivyo msaada uliotolewa leo ni sehemu ya kuisaidia na kuzalisha kiwango kikubwa cha rasilimali watu katika sekta mbalimbali hapo baadae.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...