Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

KIKOSI cha vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys tayari kimeingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya siku saba hapa nyumbani kabla ya kwenda nchini Korea Kusini kushiriki michuano ya kimataifa iliyoandaliwa na chama cha soka nchini humo.

Afisa Habari wa TFF,Alfred Lucas amesema kwamba kocha mkuu wa timu hiyo Bakali Shime tayari ameungana na timu baada ya kuwa kwenye mapumziko mafupi.

Lucas amesema kwamba safari hiyo ni ahadi ya Raisi wa TFF,Jamali Malinzi ambapo awali alidai kuwa timu hiyo licha ya kushindwa kufuzu kwa fainali za vijana zitakazofanyika nchini Gaboni lakini kikosi kitaendelea kuwepo pamoja na kitajengwa kwani nia yao vijana hao sasa wataenda kuunda timu ya Ngorongoro Heroes.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...