Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inapenda kukanusha taarifa kutoka Kwenye baadhi ya Mitandao ya Kijamii ikidai
kwamba, Mhe. Kamishna wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Balozi Omar Ramadhan Mapuri (pichani) amefariki dunia.
Taarifa
Rasmi ya Serikali kwamba taarifa hizo ni za uongo na hazina hata Chembe ya
ukweli. Mhe. Kamishna Balozi Mapuri yupo hai na afya yake iko vizuri.
Mheshimiwa
Balozi Omar Ramadhan Mapuri ambae kwa sasa ni Kamishna wa Tume ya Uchaguzi
Zanzibar alilazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa akipata
matibabu na baada ya kupata huduma kutoka kwa madaktari, Mheshimiwa Balozi
Mapuri aliruhusiwa kurejea nyumbani siku ya Jumamosi Novemba 12 baada ya afya
yake kuimarika.
Serikali
imesikitishwa na taarifa za uvumi na uzushi uliosambazwa jana na leo kwenye
mitandao ya kijamii, taarifa hizi sio za
kweli na tunawaomba wananchi wazipuuze.
Aidha,
Serikali inapenda kuvionya vyombo vya habari na Mitandao ya kijamii kuacha
kusambaza taarifa za uongo kuhusu viongozi wa Serikali.
Imetolewa
na :
Dk. Juma Mohammed Salum
Kny Mkurugenzi
Idara ya Habari MAELEZO
Zanzibar
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...