Serikali
imewataka maafisa elimu kupanga muda wa kusikiliza kero za walimu na
kuzitafutia ufumbuzi ili kuongeza morali ya walimu kufundisha. Agizo
hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe.Seleman Said Jafo alipokuwa
akiongea na walimu wa shule ya sekondari Segera iliyopo wilayani
Handeni, wakati wa ziara ya kiserikali Wilayani Handeni na Mkoa wa
Tanga.
Mhe.Jafo alisema kuwa wapo baadhi ya Maafisa elimu ambao wanajifanya kuwa ni Miungu watu linapokuja suala la kusikiliza na kutatua kero za walimu. Waziri Jafo alisema “Wapo walimu wanaotembea umbali mrefu kufuata huduma makao makuu ya Halmashauri kwa wakubwa wao mara nyingi wameshindwa kutatuliwa kero zao hali inayopelekea usumbufu, Kuanzia leo 24/11/2016 napiga marufuku tabia hiyo”.
Aliongeza
msisitizo kuwa Maafisa elimu wapo kwa lengo la kuwasikiliza walimu na
kuwasaidia kutatua kero zao ili waweze kujikita katika ufundishaji wa
wanafunzi. Alisema kuwa walimu ni watu muhimu sana nchini ila wamekuwa
wakikatishwa tamaa na utendaji wa baadhi ya maafisa elimu. Aliongeza
kuwa kero kubwa ya walimu ni kutokupanda madaraja kwa wakati na kutopata
stahiki zao ikiwa ni pamoja na posho za likizo,uhamisho na madai
mengine.
Wakati huohuo, Naibu Waziri aliiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kukamilisha miradi yote ya SEDP-II ambayo haijakamilika kuhakikisha inakamilika kabla au ifikapo tarehe 20/12/2016. Alisema kuwa katika kusimamia miradi hiyo na miradi ya maendeleo kwa ujumla kila mtu lazima atimize wajibu wake na kuhakikisha fedha iliyotengwa na kutolewa inatumika vizuri na thamani yake kuonekana kwa muda mrefu (value for money).
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Said Jafo akisaini kitabu cha wageni shule ya sekondari Segera, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Wiliam Makufwe na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe.
Picha ya pamoja ya Mhe. Selemani Said Jafo na waalimu wa shule ya sekondari ya Segera.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni akitoa utambulisho mfupi kwenye ukumbi wa Halmashauri.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.
Viongozi wakisikiliza kwa makini maagizo ya Naibu Waziri ikiwa ni pamoja na kuwa na usimamizi bora wa rasilimali fedha.
Wakati huohuo, Naibu Waziri aliiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kukamilisha miradi yote ya SEDP-II ambayo haijakamilika kuhakikisha inakamilika kabla au ifikapo tarehe 20/12/2016. Alisema kuwa katika kusimamia miradi hiyo na miradi ya maendeleo kwa ujumla kila mtu lazima atimize wajibu wake na kuhakikisha fedha iliyotengwa na kutolewa inatumika vizuri na thamani yake kuonekana kwa muda mrefu (value for money).
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Said Jafo akisaini kitabu cha wageni shule ya sekondari Segera, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Wiliam Makufwe na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe.
Picha ya pamoja ya Mhe. Selemani Said Jafo na waalimu wa shule ya sekondari ya Segera.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni akitoa utambulisho mfupi kwenye ukumbi wa Halmashauri.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.
Viongozi wakisikiliza kwa makini maagizo ya Naibu Waziri ikiwa ni pamoja na kuwa na usimamizi bora wa rasilimali fedha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...