Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga (kushoto) akisisitiza jambo wakati wa maonyesho ya wadau wa bima yaliyoandaliwa na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) yanayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya bima ya Mgen Charles Sumbwe , Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya G A Tanzania, Amit Srivastavr na Mkurugenzi Mtendaji wa kamapuni ya Bima ya Maxinsure, Bhaskar Nair. 
Mmoja wa wananchi aliyefika kwenye manesho ya wadau wa bima Gudumo Gaironga(kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga (kulia) alipokuwa akimfafanulia jambo wakati wa maonyesho ya wadau wa bima yaliyoandaliwa na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) yanayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 
Kamishina wa wa Bima Tanzania Ezraell Kamuzora (kulia) akiwapongeza wafanyakazi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wao Sam Kamanga (kushoto) wakati alipotembelea banda lao lililopo kwenye maonyesho ya wadau wa bima yaliyoandaliwa na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) yanayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga akimpongeza mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) anayesoma kozi ya maswala ya bima Baraka Dinis kwa kujitolea kutoa damu kwa ajili ya kuchangaia Mpango wa Taifa wa Damu salama kwenye maonyesho ya wadau wa bima yaliyoandaliwa na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) yanayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Elisante Maleko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...