SIMU.TV: Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad amelishutumu jeshi la polisi kuwa linatumiwa kuvuruga mikutano ya chama hicho. https://youtu.be/OGUtM-bNd1Y
SIMU.TV: Wananchi wa kijiji cha Likuyu senga Maganga mkoani Ruvuma wamechangishana nauli kwa ajili ya kutuma wajumbe kwenda kwa waziri wa ardhi kufikisha malalamiko yao ya kunyang’anywa ardhi. https://youtu.be/WmwPK90LImo
SIMU.TV: Uhaba wa mafundi wa vifaa tiba katika hospitali za rufaa na za kanda umeelezwa kuwa changamoto inayokwamisha wagonjwa kupatiwa matibabu kwa wakati. https://youtu.be/cDfcvbDUC14
SIMU.TV: Sakata la ubadhirifu wa miradi ya maendeleo jijini Dar es Salaam limeendelea kuwatikisa wenyeviti wa mitaa baada ya kuibuliwa kwa kero mbalimbali kwenye ziara ya mkuu wa mkoa huo. https://youtu.be/YtPv93XqL5U
SIMU.TV: Ukosefu wa mabeni na usafiri kwa wananfunzi wa chuo cha Ufundi stadi Veta mkoani Lindi umeelezwa kuwa changamoto inayokwamisha vijana wengi kupata mafunzo ya ufundi stadi. https://youtu.be/Ln9uJ772z0I
SIMU.TV: Serikali ya mkoa wa Shinyanga umewaagiza wakulima kulima zaidi zao la pamba baada ya kupatikana kwa soko la uhakika kwenye kiwanda cha nyuzi. https://youtu.be/MTC6GrqMK8I
SIMU.TV: Akina mama wa mji wa Mankaka wilayani Nanyumbu mkoani Mtwara wameshindwa kujitokeza kushiriki zoezi la kufanya usafi kutokana na kuhangaikia huduma ya maji. https://youtu.be/OaBlZ9JgKpc
SIMU.TV: Wadau wa michezo nchini wameiomba serikali kutengeneza miundombinu ya mchezo wa viatu vyenye matairi ili kuweza kuinua mchezo huo. https://youtu.be/nRT8yq3zIBs
SIMU.TV: Serikali imewataka vijana kutopuuza michezo mbalimbali kwa maana ni njia ya kujijengea afya bora na ajira pia. https://youtu.be/tXnFJdpapCY
SIMU.TV: Kocha mkuu wa timu ya taifa ya wanawake Sebastian Mkoma ameeleza kuwa timu hiyo itanufaika na ligi ya wanawake kwa kupata wachezaji wazuri zaidi. https://youtu.be/V8D0X63hbNo
SIMU.TV: Wachambuzi wa mpira wa miguu kutoka sehemu mbalimbali duniani wamesifu juhudi za kocha wa klabu ya Chelsea kwa kufanikiwa kuibadilisha timu hiyo kwa muda mfupi. https://youtu.be/9rNJqoLXAIM
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...