Unapo wadia mwisho wa mwaka wizi kupitia mtandao umekua ukishika kasi zaidi – Mataifa mengi duniani yamekua yakikumbwa na wimbi kubwa la uhalifu mtandao unao ambatana na upoteaji wa pesa. Itakumbukwa mwaka jana kuelekea mwisho wa mwaka ndio kirusi kipya aina ya ModPOS kilionekana kwa mara ya kwanza na kilifanikiwa kudhuru maeneo mengi na kusababisha kiasi kikubwa cha fedha kupotelea mikononi mwa wahalifu.

Mwezi huu wa kuminamoja pekee tayari kumekua na matukio mengi yenye mlengo wa kuwapatia pesa wahalifu mtandao. Kwa sasa Uhalifu mtandao kpitia kirusi cha RANSOMWARE kinachoendelea kushikakasi wamefanikiwa kupata mamilioni ya fedha. Kirusi hiki kinapelekea mhalifu mtandao kumfungia uwezo mmiliki halali kutumia kifaa chake akimtaka alipe kiasi cha pesa ili kurudishiwa huduma. Uhalifu huu umepiga hodi Barani Afrika na hadi sasa wengi wameendelea kua waathirika.

Mifumo ya hospitali, mashule na watu binafsi ni miongoni mwa waathirika wa kubwa wa uhalifu huu ambapo kila mfumo ulio fungiwa na kirusi cha Ransomware ili kufunguliwa kiasi cha dola Miatatu (300) na zaidi kimekua kiki hitajika. Kupitia matukio yaliyo ripotiwa duniani kote, takwimu halisi ya pesa zilizo ingia mikononi mwa wahalifu mtandao kwa mwezi huu wa kuminamoja pekee kutokana na Ransomware bado haija patikana ingawa ina kadiriwa kuzidi dola milioni 829.

Aidha, Mabenki nayo hayako salama – Idadi ya Mabenki yaliyo vamiwa kimtandao imeendelea kukua zaidi kuanzia mapema mwezi huu huku hali hii ikitegemewa kuendelea zaidi maeneo mengi. Tukio kubwa zaidi kwa sasa ni kutokea uingereza ambapo hadi sasa benki ya Tesco baada ya kushambuliwa kimtandao zaidi ya Paundi milioni mbili zimeweza kupotelea mikononi mwa wahalifu mtandao na benki hiyo imelazimika kuwalipa wateja wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...