Na Amina Kibwana, Globu ya Jamii
TANZANIA kufikia uchumi wa viwanda mwaka 2020 kunahitajika kuwa na
mazingira yatakayoweza kuwavutia wawekezaji watakaoweza kuwekeza viwanda ikiwa
ni pamoja na kuimarisha viwanda vidogo vidogo katika kuzalisha bidhaa kwa
wingi
Akizungumza
na Waandishi wa habari leo jijini Dar,Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa
Sekta Binafsi Nchini
(TPSF),Godfrey Simbeye ameyasema hayo wakati akitangaza mkutano wa
Kimataifa uunaotarajiwa kufanyika Desemba 5 hadi 7 katika ukumbi wa
Mwalimu Nyerere jijini Dar es
Salaam.
Simbeye amesema
kuwa mkutano huo utazishirikisha nchi mbalimbali Duniani ambazo
zimepiga hatua katika sekta ya viwanda,ambapo wawekezaji watapata fursa za kuwekeza katika sekta ya
viwanda nchini.
Mkutano
huo ambao umeandaliwa na TPSF kwa kushiriana na tasisi mbalimbali za
Serikali ikiwemo Wizara ya Viwanda,Biashara, Arusha ya International
Conference Centre, Shirika la Viwanda Vidogo, Vido IDO,TIC,EPZA,ZIPA,TTB
pamoja na TANTRADE ambapo kwa pamoja wataingaza Tanzania katika
sekta ya viwanda nchini ili iweze kuleta matunda kwa watanzania pamoja
kukuza uchumi.
Simbeye
amesema mkutano kama huo ulishafanyika mara mbili katika nchi za
Afrika ikiwepo Misri na Afrika Kusini na Tanzania imepata nafasi ya
tatu katika kufanyika mkutano huo ambapo ni fursa ya Tanzania katika
kuelekea uchumi wa viwanda kufikia 2020.
Amesema kampuni
ya Biashara nchini yatafaidika katika kutanua uwigo wa mitandao ya
kibiashara na kubadilishana uzoefu, taaluma za kuweza kufanya fursa za
uwekezaji, kuonyesha uwepo wa nchi katika jukwaa la kimataifa pamoja na
kuongeza ushawishi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kutokana na
kuongezeka mzunguko wa fedha za kigeni nchini kutokana na ujio wa
wageni wataoshiriki mkutano huo.
"Tanzania
tunajivunia kuwa nchi ya tatu katika kufanyika mkutano huu, hii ni fahari
sana kwetu, kwani tunaanza kuonekana kuwa nchi yetu ina hadhi” amesema
Simbeye.
Sembeye amesema mikutano
kama hii inapokuja katika Nchi yetu inawapa watu fursa ya kuhudhuria na
kufaidika pia inasaidia kukuza uchumi kwani tunategeme kupata wageni
400 ambapo wageni 200 watatoka nje ya nchi."
Aidha
ameongeza kuwa mkutano huo utakuwa sambamba na maonesho ya viwanda
yatakayoanza Desemba 7 hadi 11 mwaka huu ambapo washiriki wa mkutano
watapata fursa ya kutembelea maonesho hayo. Simbeye amesema Tanzania ina jumla ya viwanda 49000, lakini
viwanda vikubwa vipo 2000 tu hivyo hii ni fursa kwetu kutangaza bidhaa
zetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...