Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Katibu mkuu wa Wizara ya habari  Sanaa na michezo Profesa Elisante Ole Gabriel amesema kuwa tatizo la ukosefu  wa ajira Afrika ni matokeo na sio tatizo kama watu wanavyosema ama dhania.

Profesa Gabriel amesema hayo katika Mdahalo wa wanazuoni  kutoka Afrika Mashariki uliofanyika katika ukumbi wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.

"Tatizo kubwa la Afrika ni soko na kubadilisha fikra za vijana katika bara letu kwa  kupata ellimu juu ya namna   Watakavyoweza kujikwamua kiuchumi  hali itakayosadia kuondokana na umaskini uliokithiri hivyo ifike hatua watu wasiwe wanahitaji kupewa pesa pindi inapohitaji kupewa elimu "amesema Profesa Gabriel

Amewataka wakufunzi wa vyuo kurudi vyuoni na kubadilisha mawazo ya vijana kurudi katika mtazamo chanya wa kujipatia maendeleo kuliko kusubiri kusukumwa na watu juu ya kupata ajira.
 Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza katika Mjadala huo
washiriki wakimsikiliza Profesa Ole Gabriel

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...