Na Editha Karlo,Globu ya Jamii -Saadani

UMOJA wa waandishi habari wanawake Tanzania(WJT)wameanza ziara ya utalii wa ndani na ya kazi katika hifadhi ya Taifa ya Saadani.

Ziara hiyo ya siku kumi iliyofadhiliwa na SHIRIKA la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA)ambayo imehusisha wanahabari wanawake kutoka mikoa mbalimbali nchini wa vyombo mbalimbali wanavyofanyia kazi.

Akiongea na mtandao huu mwenyekiti wa umoja huo wa wanahabari wanawake Ester Macha mwandishi wa gazeti la majira kutoka Mkoa wa Mbeya alisema kuwa ziara hiyo itawapa fursa ya kujifunza na kuona kwa vitendo vivutio mbalimbali vilivyopo katika hifadhi za Taifa watakazo tembelea.

"Tumefurahi sana ka wanahabari kupata fursa hii ya kutembelea hifadhi zetu ikiwa ni sambamba na kuzitangaza kupitia kalamu zetu"alisema Ester.Aliwataka wananchi wote kujenga tabia ya kutembelea hifadhi zetu nasi kuwaachia wageni kutoka nje peke yao kuja kutembelea hifadhi na kufanya utalii.

Naye Mhifadhi utalii wa hifadhi ya Taifa ya Saadani Hapaikunda Mungure alisema hifadhi ya saadani ina utalii wa kuangalia wanyama kwa kutembea na magari,fukwe nzuri za bahari,utalii wa boti kwenye mto wami,matembezi ya miguu.
Mhifadhi utalii wa hifadhi ya Taifa ya Saadani Apaikunda Mungure akitoa maelezo mafupi kwa waandishi wa habari wanawake kuhusu utalii wa boti unaofanywa ndani ya mto wa wami katika hifadhi ya saadani.

Mwandishi wa habari wa blog hii Editha Karlo(kushoto)kutoka Kigoma na mwandishi wa gazeti la mwananchi Joyce Joliga kutoka Mkoa wa Ruvuma wakifanya utalii wa boti ndani ya mto wami uliopo hifadhi ya Taifa ya saadani.
Waandishi wa habari wanawake kutoka mikoa na vyombo mbalimbali wakifanya utalii wa ndani wa boti kati mto wami ndani ya hifadhi ya Saadani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...