UMOJA
wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wamejiunga pamoja kuendesha
kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini
Tanzania . Aidha kwa pamoja wamezuru miradi iliyofadhiliwa na EU. Wakiwa
Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka
vyuo vikuu vya Iringa na Mkwawa kwenye semina iliyoelezea malengo hayo
ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani.
Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania.
Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ripoti na makabrasha
mbalimbali ya Umoja wa Mataifa mara baada ya kuhitimisha semina kuhusu
SGDs kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mwongoza
wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Deonis Mgumba akitoa
maelezo ya vifaa mbalimbali vilivyokuwa vikitumika enzi za utawala wa
kichifu kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro
Rodriguez (kushoto) na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa
Iringa, Henry Mditi (katikati) walipotembelea makumbusho hayo mjini
Iringa.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi
wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro
wakitwanga mahindi kienyeji katika moja ya kinu kilichokuwa kinatumika
enzi hizo za utawala wa kichifu kilichopo katika makumbusho hayo.
Mwongoza
wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Matatizo Kastamu akitoa
maelezo ya picha mbalimbali zenye kumbukumbu za utawala wa kichifu na
historia ya mji wa Iringa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa
Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa
(UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya
(EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mwakilishi
wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro
(kushoto), Mtalaam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu
na Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever wakipitia vipeperushi
vyenye maelezo ya kina ya Mradi wa Fahari Yetu unaoendesha Makumbusho na
Kituo cha Utamaduni mkoa wa Iringa.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi
wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro
katika picha ya pamoja kwenye sanamu maalum za mavazi ya kipindi cha
utawala wa Chifu Mkwawa walipotembelea Makumbusho ya mkoa wa Iringa.
HABARI ZAIDI SOMA HAPA
HABARI ZAIDI SOMA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...